AJALI YAUA WEZI MGODI WA DHAHABU WA GGM


Watu wawili wamekufa kwa kufukiwa na kifusi cha mawe katika Mgodi wa Dhahabu wa GGM watu hao wameingia mgodini humo kwa kinyume na sheria kwa lengo la kuiba mawe ya dhahabu.

Tukio hilo limetokea july 30 majira ya jioni ambapo watu wawili mmoja mkazi wa Nyamalembo na mwingine nyankumbu kwa nyakati tofauti wameingia katika moja ya mashimo mgodini humo na bahati mbaya mawe yakadondoka na kufukia.

katika tukio la july 30 uongozi wa GGM baada ya kupata taarifa ya kufukia kwa watu wamelijulisha jeshi la polisi na ofisi ya madini na kuja eneo la tukio na kufanikiwa kuwatoa watu wawila na mmoja alifariki na mwingine akiwa katika hali mbaya na alipelekwa hospitali ya wilaya na hatimaye kufariki july 31 saa 4 asubuhi.

Ni mmoja wa Walinzi wakiwataka vijana kutoka katika maeneo hayo ili kupisha mlipuko unaotakiwa kufanyika lakini vijana hao walikaidi na kubaki katika mashimo.Ni vijana wengi wakiwa chini ya umri wa miaka 18 huingia mgodini kupitia katika milima ambayo ni hatari kwa usalama wao na eneo hili limepewa jina na vijana hao maaa rufu kwa jina la Magwangara kwa kuitwa Kaza Roho.

Mkuu wa Ulinzi GGM Peter Marwa amesema vijana wengi usiku na mchana wanaingia kila siku na kwa wingi wao inawawia vigumu kuwadhibiti hivyo hutumia busara kuwaondoa maeneo ya hatarishi lakini vijana hao wanajificha katika mashimo.

Kutokana na kutokea kwa matukio haya mara kwa mara Mkuu wa wilaya ambaya ni mwenyekiti wa kamati ya ulinzi na usalama Manzie Mangochie akiandamana na waandishi wa habari kuona eneo la tukio na njia wanazopita vijana wa magwangala na kusema jamii lazima ibadilike kwa kuona hatari inayowakabili vijana na matukio yakitoke lawama za moja kwa moja zinauendea Mgodi.

Mkuu huyo ameongeza kuwa ni vyema viongozi wa vitongoji kuwa na ulinzi shirikishi ili iwe njia ya kudhibitiana kwakua vijana hao wanaishi maeneo yao huku Afisa madini Mkazi Haruna Sementa akijikita kuzungumzia sheria zaidi.
CHANZO:STAR TV HABARI


JIUNGE NA EDMO BLOG SASA

Usipitwe!! Jiunge nasi kupitia Facebook,Twitter na Instagram ili kupata habari zote za town! Usikose kujiunga na Youtube kuangalia video zote kali kutoka Edmo Blog Pekee!, kujiunga bonyeza hapa>>>Youtube

Tupe Maoni Yako lakini Usiandike Matusi



 
© Copyright EDMO BLOG | Designed By Peruzibongo