AJALI YA GARI ENEO LA MINDU MKOANI MOROGORO





Gari aina ya ya lsuzu lenye namba za usajili T 749 CCG baada ya kupata ajali eneo la Mindu mkoani Morogoro.
 
GARI aina ya Isuzu yenye namba za usajili T749 CCG lililokuwa likisafirisha nyanya kutoka kijiji cha Mlali kuelekea kwenye moja ya masoko ya mji wa Morogoro jana mchana lilipata ajali na kupinduka eneo la Mindu jirani na bwawa la Mindu mkoani hapa.
 
Mashuhuda wa tukio hilo walidai kwamba gari hilo lilipinduka baada ya kujaribu kumkwepa mwendesha bodaboda na kwamba katika ajali hiyo hakuna mtu aliyepoteza maisha ingawa baadhi ya wamiliki wa mizigo iliyokuwemo katika gari hilo walijeruhiwa.
 
'Unajua hivi vigari ni vyepesi sana hivyo kikiyumba kidogo tu kinapinduka, wafanyabiashara kwa kawaida huwa wanakaa juu ya matenga yao lakini kwenye tukio hili wamiliki wa matenga hayo ya nyanya walikaa kwa dereva, sipati picha kama wangekaa juu ya matenga yao kama ilivyozoeleka siku zote" alisema shuhuda huyo aliyejitambulisha kwa jina la Johnson Joseph.
 
(Picha / Habari na Dustan Shekidele GPL, Morogoro


JIUNGE NA EDMO BLOG SASA

Usipitwe!! Jiunge nasi kupitia Facebook,Twitter na Instagram ili kupata habari zote za town! Usikose kujiunga na Youtube kuangalia video zote kali kutoka Edmo Blog Pekee!, kujiunga bonyeza hapa>>>Youtube

Tupe Maoni Yako lakini Usiandike Matusi



 
© Copyright EDMO BLOG | Designed By Peruzibongo