Mzee Ezekia Sanga akiwa na mkewe Ester Mbilinyi baada ya kufunga ndoa
mzee simon akifunga ndoa na mkewe Emeliana Mahenge
kanisa walilotumia kufungia ndoa
Wananchi wa kijiji cha Maleutsi wilaya ya Makete mkoani
Njombe hii leo wameshuhudia tukio la aina yake la vikongwe wawili kufunga pingu
za maisha(harusi) tukio linalodaiwa kuwashangaza wengi na kuweka historia
katika kijiji hicho
Harusi hiyo iliyofanyika katika kanisa katoliki Maleutsi
limeshuhudiwa na umati mkubwa wa watu, ambapo wazee hao wanaokadiriwa kuwa na
zaidi ya miaka 70 limehusisha ndoa mbili kati ya Ezekia Chaula na Ester
Mbilinyi na nyingine ya Mzee Simon na Emeliana Mahenge wote wakazi wa kijiji
hicho
Wakizungumzia tukio hilo wananchi wa kijiji hicho wamesema
si kawaida kushuhudia tukio kama hilo na kuongeza kuwa hayo yaliyotokea
yamekuwa fundisho kwa wengine hasa vijana ambao wanadhani suala la kufunga ndoa
haliwezekani
“Ama kwa hakika hii ni ajabu kwa kweli maana wazee kama hawa
wenye wajukuu na vitukuu kufunga harusi, maana wao wameshazeeka na hawana haja
hiyo tena na hata wasingefanya hivyo hakuna wa kuwauliza maana umri umekwenda,
kwa kweli hii ni ajabu lazima sisi kama vijana tujifunze” alisema Eliza sanga
Tukio hilo linadaiwa kuweka historia kubwa katika kijiji
hicho na wilaya ya Makete kwa ujumla