WANAKIJIJI WAFANYA MAOMBI KUJITAKASA KUFUATIA TUKIO LA KUBAKWA KWA PUNDA HADI KUFA KIJIJINI HAPO

Punda
WAKAZI wa kijiji kimoja Kaunti ya Murang’a ambapo inashukiwa punda alibakwa hadi kufa walifanya maombi mnamo Jumatano hii ili kujitakasa.
Wakiongozwa na wahubiri kutoka makanisa kadhaa kutoka sehemu hiyo, wakazi wa kijiji cha Nyati, Lokesheni ya Kamahuha katika eneo bunge la Maragua walikashifu kitendo hicho na kumwomba Mungu msamaha.

Mhubiri Joseph Kamande wa dhehebu la Akorino eneo la Kamahuha alilinganisha kitendo hicho na miji ya Sodoma na Gomorrah katika Kitabu cha Mwanzo kwenye Biblia.

“Hili ni jambo la kushangaza na tunafaa kuomba Mungu atusamehe, hatutaki kijiji chetu kiwe kama Sodoma na Gomorah,” alisema Mhubiri Kamande akiwahutubia wakazi katika uwanja wa Nyayo ambapo kulitokea kisa hicho.

Inadaiwa wanamme ambao idadi yao haijulikani walimchafua punda huyo wa kiume hadi akafa wakati wa usiku.

Mnyama huyo wa thamani ya Sh15,000 aliyekuwa anamilikiwa na Bw Peter Murigi alipatikana akiwa amefungiliwa chini ya mti wa mwembe akiwa amekufa katika uwanja wa Nyayo huku mipira 10 ya kondomu ambayo ilikuwa imetumiwa ikiwa imetapakaa mahali hapo.

Kesha
Cha kushangaza ni kuwa kisa hicho kilitokea mita chache tu kutoka kwa kanisa moja ambapo maombi ya kesha yalikuwa yanafanyika.

“Hatujui ni shetani mgani amewashika wanamme wetu na sote tuko hatarini ya kunajisiwa na waliochafua punda huyo,” alisema Bi Esther Muthoni huku majonzi ya huzuni yakimtoka.

“Hizi ni siku za mwisho ambazo zilitabiriwa na manabii wa Biblia na tunaomba Mungu atusaidie,” alilia Bi Muthoni.
Na SAMUEL KARANJA


JIUNGE NA EDMO BLOG SASA

Usipitwe!! Jiunge nasi kupitia Facebook,Twitter na Instagram ili kupata habari zote za town! Usikose kujiunga na Youtube kuangalia video zote kali kutoka Edmo Blog Pekee!, kujiunga bonyeza hapa>>>Youtube

Tupe Maoni Yako lakini Usiandike Matusi



 
© Copyright EDMO BLOG | Designed By Peruzibongo