WANAFUNZI WA SEKONDARI YA JUNIOR SEMINARI MOROGORO WAANDAMANA

 
Wanafunzi wa shule ya sekondari ya Junior Seminari inayomilikiwa na kanisa la KKKT jimbo la Morogoro  wamefanya mgomo wa kutoingia darasani na  kufanya maandamano kwenda ofisi za askofu kuukataa uongozi wa shule kwa madai kushindwa kuweka huduma muhimu  za taaluma na kuajiri walimu wasio  na uwezo wa kufundisha hali inayosababisha kushuka kwa kiwango cha taaluma katika shule hiyo.

Ndivyo walivyosikika wanafunzi hao wakiimba nyimbo za dini wakiandamana kuelekea katika kanisa la KKKT mji mpya huku askari wa jeshi la polisi wakiyasimamisha maandamano kwa muda hadi alipofika askofu wa jimbo la Morogoro Jacob Mameo ambapo maandamano yalielekea kanisani na kabla ya mazungumzo kuanza walianza maombi kisha wanafunzi wakakabidhi malalamiko yao kwa maandishi ambapo akijibu malalamiko hayo askofu Maleo ameahidi kuyafanyia kazi ikiwemo kuitisha kikao cha bodi ya shule kwa haraka.

Muda wote wanafunzi walionekana kutokuridhika na majibu ambapo wameeleza kuwa malalamiko yao ni ya muda mrefu na kubwa wanalolalamikia ni uwezo mdogo wa baadhi ya walimu katika kufundisha na jingine wakilalamikia urasimu wa mwalimu mkuu wa shule hiyo Laison Saming'o kushindwa kusimamia upatikanaji wa huduma za afya,vifaa vya shule na usimamizi mbaya wa mitihani.

Nae katibu tawala wa wilaya ya Morogoro Sulpius Mlenge akizungumza kwa niaba ya mkuu wa wilaya ya Morogoro ameomba askofu kutafuta ufumbuzi wa haraka wa malalamiko ya wanafunzi hao ili yasiathiri taaluma zao na  kuwasihi wanafunzi kutulia ambapo baadae wanafunzi hao walirudishwa shuleni kwa daladala.

CHANZO:ITV


JIUNGE NA EDMO BLOG SASA

Usipitwe!! Jiunge nasi kupitia Facebook,Twitter na Instagram ili kupata habari zote za town! Usikose kujiunga na Youtube kuangalia video zote kali kutoka Edmo Blog Pekee!, kujiunga bonyeza hapa>>>Youtube

Tupe Maoni Yako lakini Usiandike Matusi



 
© Copyright EDMO BLOG | Designed By Peruzibongo