VIJANA MKOANI IRINGA WATAKIWA KUSHIRIKI AFYA YA UZAZI

VIJANA mkoani Iringa wametakiwa kushiriki katika afya ya uzazi kwa vijana ili kuzijua na kuzitambua haki za afya ya uzazi kwa vijana na kutambua mahitaji yao muhimu.

Akizungumza leo,Ofisa utetezi na sera wa mradi wa haki ya afya ya uzazi kwa vijana Meshack Mollel alisema kuwa vijana wanatakiwa kushiriki na kupata elimu ya afya ya uzazi ili kujitambua na kujua haki zao na kuunda sera zinazowahusu.

Mollel alisema kuwa mradi huu unatekelezwa katika manispaa tatu ikiwamo  IRinga , Ilala na Kinondoni ili kutoa elimu ya afya ya uzazi kwa vijana kwa kushirikiana na  shirika la afya na tiba  AMREF chini ya ufadhili wa shirika maendeleo la nchini  swedeni(SIDA).

“Tamasha hili la vijana lenye kauli mbiu inayosema “hamasisha ushiriki wa vijana ili kutambua mahitaji muhimu katika afya ya uzazi”pia tukiwa na lengo la kutoa elimu na kuzijua haki  za afya ya uzazi kwa vijana na kuwapa fursa ya kuunda sera zinazo wahusu vijana”alisema Mollel.

Kwa upande wake naibu meya wa manispaa ya Iringa Gervas Ndaki ambaye alikuwa mgeni rasmi alisema kuwa anafurahi kuwaona vijana wamejitokeza kwa wingi hivyo anaimani hata katiba mpya ya sasa itakuwa na maoni na sera zinazo muhusu kijana.

“dhana hii ya michezo ni dhana nzuri ya kuwakutanisha vijana kwa sababu kwanza michezo inapendwa na vijana wengi na  inajenga afya zao na kuwa fanya waondokane na makundi yasiyofaa kutokana na vijana kuwa na changamoto nyingi”alisema Ndaki.


JIUNGE NA EDMO BLOG SASA

Usipitwe!! Jiunge nasi kupitia Facebook,Twitter na Instagram ili kupata habari zote za town! Usikose kujiunga na Youtube kuangalia video zote kali kutoka Edmo Blog Pekee!, kujiunga bonyeza hapa>>>Youtube

Tupe Maoni Yako lakini Usiandike Matusi



 
© Copyright EDMO BLOG | Designed By Peruzibongo