Muonekano wa Choo cha soko la Lupila kwa nje.
Muonekano wa choo cha soko la Lupila kwa ndani.
Wafanya
biashara na wateja waliokuwa mnadani katika kata ya Lupila wilayani Makete
mkoani Njombe hii leo wamelalamikia uchafu wa vyoo vya soko hilo, uliosababisha kero kwao huku wengine
wakikwepa kwenda kujisaidia kwenye vyoo hivyo
Wakizungumza
na mtandao huu mnadani hapo wamesema hali hiyo imekuwa tofauti na sehemu
nyingine walizotembelea wilayani hapa na kufanya minada ambapo wanakuta vyoo
vikiwa katika hali ya usafi, lakini waliyokutana nayo mnadani hapo hii leo ni
hatari
Mmoja
ya mfanyabiashara aliyejitambulisha kwa jina la Bi. Nesfaneti Digati amesema
wahusika hawajajipanga vizuri katika hali ya usafi wa vyoo na hali hiyo
inaonesha si kwamba imetokea leo tu bali vyoo hivyo havifanyiwi usafi kwa muda
mrefu
“Tunajua
Makete kwenye sehemu zote tulizopitia vyoo vinakuwa safi, mfano Ikonda, Makete na hata Kidope
lakini hapa leo tumefika kwa mara ya kwanza kufanya mnada lakini hii ya leo
hairidhishi kabisa” alisema Bi. Digati
Kwa
upande wake Beni Sanga amesema anashangazwa na hali hiyo ya uchafu wa vyoo
mnadani Lupila, na kusema endapo hali hiyo haitafanyiwa kazi haraka
iwezekanavyo upo uwezekano wa kuwepo magonjwa ya milipuko ikiwemo kipindupindu
Mtandao
huu umefika kujionea hali ya vyoo hivyo na kuvikuta vikiwe vimekithiri uchafu, huku
wengine wakijiendea vichakani kujisaidia kutokana na hali mbaya ya vyoo hivyo
Akizungumzia
hali hiyo Afisa mtendaji wa kata ya Lupila Bw. Antony Solomoni Seso amekiri
kuwepo kwa hali hiyo na kusema walikuwa wamepanga kufanya kikao na halmashauri
ya kijiji kuona namna ya uendeshaji wa vyoo hivyo lakini haikuwezekana kutokana
na mjumbe wa halmashauri ya kijiji kufariki siku ya kikao hivyo kuahirisha
Amesema
wakiwa kwenye utaratibu wa kufanya kikao kingine ndipo wakapata taarifa za
mnada huo kabla ya kulifanya hilo, lakini
ameongeza kuwa watakaa mara moja kulitatua suala hilo