RPC IRINGA AKEMEA VITENDO VYA UBAKAJI VILIVYOSHIKA KASI MKOANI MWAKE

Kutokana na vitendo vya ubakaji kushamiri katika mkoa wa Iringa, Kamanda wa jeshi la polisi RAMADHANI MUNGI amekemea vikali vitendo hivyo na kusema kuwa ni makosa dhidi ya Binadamu.
Akizungumza,Kamanda  Mungi amesema kuwa mtu yoyote anayefanya mapenzi na msichana au binti chini ya umri wa miaka 18 hata kama atakuwa amekubali kwa hiari yake bado atahesabiwa kuwa mbakaji.
 
Mungi amesema kuwa vitendo hivyo vinasababishwa na matatizo ya kisaikolojia hivyo watalamu wa saikolojia wanapaswa kulishugulikia suala hilo ili kusaidia kupunguza matukio kama hayo.
 
Aidha ameongeza kwa kusema kuwa kutokana na wananchi wengi kulalamika juu ya kuachiwa huru kwa watuhumiwa wenye makosa ya ubakaji, amesema kuwa ni haki yao kupewa dhamana kwa mujibu wa sheria na sio kwamba polisi wanafanya makusudi.


JIUNGE NA EDMO BLOG SASA

Usipitwe!! Jiunge nasi kupitia Facebook,Twitter na Instagram ili kupata habari zote za town! Usikose kujiunga na Youtube kuangalia video zote kali kutoka Edmo Blog Pekee!, kujiunga bonyeza hapa>>>Youtube

Tupe Maoni Yako lakini Usiandike Matusi



 
© Copyright EDMO BLOG | Designed By Peruzibongo