
Mkazi wa kijiji cha Mwalisi
kata ya Ngana wilayani Kyela Mkoani Mbeya Enita Kalota (23)amekutwa amekufa
katika maeneo ya Kitongoji cha Kandete kijiji cha Ngana huku akiwa amenyofolewa baadhi ya viungo
katika mwili wake,
Akizungumza na Ripota wetu ofisini kwake kaimu ofisa
mtendaji wa kata hiyo ya Ngana Joseph Mapunda alidai kuwa ofisi yake ilipata
taarifa ya kuwapo mtu aliyeuawa katika kijiji hicho cha Ngana mnamo majira ya
saa 3 asubuhi jana na baada ya hapo walitoa taarifa kituo kidogo cha Polisi cha
Kasumulu,
Alisema msichana huyo alikuwa anaishi Boda ya Kasumulu baada ya
kumaliza shule darasa la saba miaka ya hivi karibuni katika shule ya msingi Mwalisi alianza kufanya shughuri za kuuza
vinywaji kwenye baa na kuwa jana walishangazwa baada ya kuuona mwili wa
msichana huyo akiwa amefia katika kijiji cha Ngana,
Mapunda alifafanua kuwa mbali na kuwepo kwa tukio hilo
hakufanikiwa kuuona mwili huo na kuwa anasubiri kuletewa ripoti kutoka kwa
afisa mtendaji wa kijiji ili aziweke katika kumbukumbu ambapo wakazi wa eneo
hilo waliouona mwili huo wanadai kuwa walivyoutizama
mwili wa mwanamke huyo walikuta baadhi
ya viungo vyake vikiwa havipo kama sikio, ngozi ya kisogoni vikiwa imeondolewa
huku kukikwa na tetesi kuwa hata sehemu zake za siri nazo zimeondolewa,
Kwa upande wake mwenyekiti wa kijiji cha Ngana Stanley
Shimwela alisema kuwa tukio hilo limewashitua sana wananchi wa kijiji hicho
ukichukulia hilo ni tukio la tatu kwa mwaka huu wa 2013 ambapo vifo vyote
uhusishwa na imani za kishirikina baada ya maiti zote zilizouawa kunyofolewa
baadhi ya viungo vya mwili,
Mganga wa zamu katika hospitali ya wilaya Kyela aliyeufanyia
uchunguzi mwili huo Dkt,Nsubiri Mwansule alisema kuwa baada ya wao kuufanyia
uchunguzi mwili huo walibaini msichana huyo kupigwa na kitu chenye ncha kali
eneo la kisogoni kichwani kilichopelekea maumivu makali na kupelekea kifo cha
mwanamke huyo,
Alisema kuwa hawezi kusema lolote juu ya kutokuwepo kwa baadhi ya
viungo ambavyo havipo katika mwili wa marehemu kwa madai kuwa yeye si mmsemaji
wa hospitali hiyo,
Kaimu mganga mkuu wa hospitali ya wilaya Dkt Apaisaria Rumisha
alipotafutwa ili kulitolea ufafanuzi jambo hilo hakuweza kupatikana kwa madai kuwa yupo
katika ofisi za halmashauri ya wilaya kwenye kikao.
Jeshi la polisi Wilayani hapa waliruhusu familia ya marehemu
kuendelea na taratibu za mazishi baada ya mwili huo kufanyiwa uchunguzi huku
wao wakiendelea na uchunguzi wa kuwabaini wahusika wa tukio hilo,
Wananchi kwa
upande wao wameiomba kamati ya ulinzi na usalama ya Wilaya ya Kyela kufanya
juhudi za haraka za kuhakikisha wanakemea vitendo hivyo ili kuweza kupunguza
vitendo hivyo vya mauaji vinavyotokea kwa imani za kishirikina vinavyoipa sifa
mbaya Wilaya ya Kyela,
Wamesema
kuwa Mkoa wa Mbeya unaongoza kuwa na makanisa mengi
ukilinganisha na mikoa mingine ambapo kila kata kuna zaidi ya makanisa matano
lakini ndiyo Mkoa wa kwanza kuwa na matukio mengi yanayohusishwa na imani za
kishirikina na biashara haramu za kuuza viungo vya binadam.
Na Ibrahim Yassin