MTUHUMIWA WA UHALIFU AJISALIMISHA MWENYEWE POLISI BAADA YA KUSAKWA KWA MIEZI MITATU

 Magari ya polisi
NA DANIEL NYASSY.
MSHUKIWA wa ulanguzi wa mihadarati Jumanne alijisalimisha kwa utawala wa kaunti ya Mombasa baada ya kusakwa kwa mda wa miezi mitatu.
Afisa mkuu wilayani Jomvu Bw Kennedy Gitonga alisema kwamba Bw Hassan Babu anayeshutumiwa kwa uuzaji wa kokeni na heroini eneo zima la Jomvu alijisalimisha mbele ya wazee wa mtaa na naibu wa Chifu wa Miritini Bw Kombo Matano.

Wananchi walilalamika vikali kwamba Bw Babu alikuwa akilindwa na maafisa fulani wa polisi aliokuwa akiwalipa.

“Ilionekana kwamba ni kweli mtuhumiwa alilindwa na polisi kwa sababu ilikuwa vigumu kumkamata na hata tulipomshika, alitoroka kutoka korokoroni kwa njia ya kiajabuajabu,” alithibitisha Bw Gitonga.

Alisema ilimbidi kuuandikia barua utawala wa kaunti pamoja na wakuu wa polisi kuwapa makataa ya siku saba kumtoa Bw Babu  “ama sivyo kungewaka moto," alisema.

Bw Babu alijitokeza ndani ya muda huo wa makataa. Alikwenda kwa wazee na naibu wa chifu na kutia saini kuapa kwamba ataachana na biashara hiyo haramu.

“Aliletwa kwangu ambako pia alitoa ahadi kama hiyo na kutia saini stakabadhi Fulani. Sasa tunamtumia na anatusaidia kuwasaka wengine aliokuwa akifanya biashara nao,” alisema Bw Gitonga

Mbunge wa eneo hilo la Jomvu Bw twalib Badina muwakilishi wa wodi Bw Karisa Nzai wamejitolea kumpeleka Bw Babu kwenye kituo cha kurekebisha wahusika wa dawa za kulevya, aliongeza Bw Gitonga.

Vilevile, watengenezaji wa pombe haramu ya chang’aa na wauzaji zaidi ya 50 wamejisalimisha kwa mkuu huyo wa tarafa huyo kwa mda wa wiki mbili, alisema Jumanne.

Misako
“Hii ni kufuatia elimu nyingi kwa jamii vijijini, kwenye mabaraza na hafla nyingine. Pia, tumeweka mkazo na misako ya mara kwa mara kwa hivyo, wafanyabiashara hiyo haramu wameona hawana pa kukimbilia,” alisema Bw Gitonga.

Miongoni mwa waliojisalimisha ni 20 kutoka kijiji cha Miritini Station, 20 kutoka kijiji cha Kwa Matee, 15 kutoka kijiji cha Bahati na wengine kutoka mtaa duni wa Bangladesh.

“Pia tumehusisha sana shirika la Nacada na kitengo cha mvinyo kwenye vita hivi. Tunawataka wahusika waache biashara hii na kujihusisha na biashara mbadala,” alisema Bw Gitonga.

“Tunawataka waanzishe biashara haramu. Tumewataka wajiunge kwenye makundi ya 10-20 na watafute mahali pa kufanya biashara halali na tutawasaidia,” alisema Bw Gitonga.


JIUNGE NA EDMO BLOG SASA

Usipitwe!! Jiunge nasi kupitia Facebook,Twitter na Instagram ili kupata habari zote za town! Usikose kujiunga na Youtube kuangalia video zote kali kutoka Edmo Blog Pekee!, kujiunga bonyeza hapa>>>Youtube

Tupe Maoni Yako lakini Usiandike Matusi



 
© Copyright EDMO BLOG | Designed By Peruzibongo