Baadhi ya
wakazi wanasema waliwaona wanaume hao wanne wakimfunga kamba mnyama huyo
lakini hawakuwa wakifahamu waliyopanga kutekeleza.
Inadaiwa kuwa
mipira ya komdomu iliyotumika ilipatikana baadaye eneo ambalo tukio
linadaiwa kutekelezwa, ishara kwamba walikuwa wamejiandaa.
Mwakilishi wa
Wodi Gitau Njoroge alitaja kitendo hicho kuwa cha kushangaza na cha
kishetani na kuwataka polisi waharakishe uchunguzi.
“Wanawake
eneo hili wanalalamika kwamba wananyimwa haki zao katika ndoa kutokana
na ulevi. Vitendo kama hivi sharti vilaaniwe na wote,” akasema.
Punda huyo anadaiwa kufariki kwa kukabwa koo na kunyimwa hewa.
Kwingineko, mwanamume alishtakiwa mjini Nyeri kwa kumchafua kuku.
Dhamana
Paul Nderitu
Kihia alikanusha shtaka la kumchafua kuku Julai 18, kijiji cha Kigwadi,
Kaunti ya Nyeri na akaachiliwa huru kwa dhamana ya Sh100,000 na mdhamini
wa kiasi sawa.
Polisi
waliambia Hakimu John Aringo kuwa mshtakiwa alifumaniwa akitenda kitendo
hicho na mwanawe wa kiume wa umri wa miaka 10 ambaye alimpasha habari
kakake mkubwa na kwa pamoja wakaripoti kisa hicho kwa chifu na mshukiwa
akakamatwa.
Kuku huyo
anayedaiwa kumilikiwa na mwanawe mkubwa wa mshukiwa alichukuliwa na
polisi kama ushahidi lakini akafariki baadaye. Mzoga wake ulikabidhiwa
afisa wa matibabu ya mifugo kwa uchunguzi kubaini chanzo cha kifo. Kesi
hiyo itasikizwa tena Agosti 20.