Na Saimeni Mgalula
Mama Roida Mparagate (37) mkazi wa kijiji cha igawa kilichopo wilaya ya mbarali mkoani mbeya amejifungua watoto wanne juzi.
Akizugumza na mwandishi kwa njia ya simu mmoja wa mashuhuda,Batoni Mbuna alisema mtoto wa kwanza alijifungulia nyumbani mnamo saa 3 asubuhi na wengine watatu alijifungulia katika hospitali ya wilaya hiyo mnamo saa 3 usiku.
Mbuna alisema kwa bahati mbaya wototo hao wote walifariki usiku huo huo na mazishi yalifanyika jana mnamo saa 9 Alasiri.