HARAMBEE YA KITUO CHA UDIAKONIA TANDALA MAKETE YAKUSANYA ZAIDI YA MILIONI 8

Mkuu wa wilaya ya Mbeya Dk Norman Sigala akizungumza kwenye harambee hiyo.

Zaidi ya shilingi milioni 8 zimepatikana katika harambee ya kuchangia sehemu ya mradi wa ujenzi wa nyumba mpya ya kulala wageni inayotarajiwa kugharimu sh. milioni 150 katika kituo cha Udiakonia Tandala kilichopo kata ya Tandala wilayani Makete mkoani Njombe mwishoni mwa wiki

Kituo hicho ambacho kipo chini ya kanisa la kiinjili la kilutheri Tanzania (KKKT) dayosisi ya kusini kati kimefikia hatua hiyo kama njia mojawapo ya kujipatia mapato ili kiweze kujiendesha chenyewe

Mgeni rasmi katika harambee hiyo mkuu wa wilaya ya Mbeya Dk. Norman Sigala alichangia kiasi cha shilingi milioni 2 kutokana na kuona umuhimu wa mradi huo ambao unatarajiwa kuwa chachu ya maendeleo ya kituo hicho

Dkt Sigala pamoja na mambo mengine pia amewaasa viongozi wa dini kutojihusisha na masuala ya kisiasa kwa kuwa dini na siasa havikai pamoja na matokeo yake kutaliletea matatizo taifa letu

"Ndugu zangu, dini na siasa haviendani kamwe viongozi wa dini nawaomba msijihusishe na masuala ya siasa kwani hayakai pamoja, ili kuepuka migogoro isiyo ya lazima hapa nchini" alisema Dk sigala

Kwa upande wake Katibu wa kituo hicho mdiakonia Elikana Kitahenga ametoa wito kwa wananchi wa wilaya ya makete ambao wanafanya kazi nje ya wilaya hiyo kuona umuhimu wa kuchangia shughuli za kiamendeleo katika wilaya hiyo kwa kuwa hakuna atakayefanya maendeleo kwenye wilaya yao isipokuwa wao wenyewe

Amesema wilaya hii pamoja na kujengwa na watu wengine lakini zaidi maendeleo yatafanywa na wanamakete wenyewe bila kujali wapo ndania ama nje ya wilaya hiyo

Na Ergon Sanga


JIUNGE NA EDMO BLOG SASA

Usipitwe!! Jiunge nasi kupitia Facebook,Twitter na Instagram ili kupata habari zote za town! Usikose kujiunga na Youtube kuangalia video zote kali kutoka Edmo Blog Pekee!, kujiunga bonyeza hapa>>>Youtube

Tupe Maoni Yako lakini Usiandike Matusi



 
© Copyright EDMO BLOG | Designed By Peruzibongo