Matokeao ya uchaguzi katika kata nne
za jiji la Arusha ambazo zote zimechukuliwa na Chama cha demokrasia na
maendeleo Chadema yamepokelewa kwa shangwe na furaha kubwa na viongozi
na wanachama wa chama hicho.
Miongoni mwa viongozi waliozungumzia matokeo hayo ni pamoja na
mbunge wa jimbo la Arusha Mh Godbless Lema ambaye amesema matokea hayo
pamoja na kuwapa wananchi wa Arusha nafasi kubwa ya kuleta mabadiliko
yametoa mwelekeo mpya wa Chama hicho katika harakati zake za kuongoza
nchi uchaguzi ujao.
Katika uchaguzi huo uliofanyika kwa amani ukihusisha kata za
kaloleni themi , kimandolu, na elerai pamoja na kufanyika kwa amani na
utulivu mkubwa huku ulinzi ukiwa umeimarisha kila kona katika vituo vya
uchaguzi, vituo vya kuhesabu kura na kona mbalimbali za jiji la Arusha
changamoto kubwa ilikuwa ni idadi ndogo ya watu waliojitokeza kupiga
kura ikilinganishwa na Waliojiandisha.
Baada ya kutangazwa kwa matokeo hayo ya madiwani wapya wa kata zote
nne ikiwemo ya Kaloleni inayoongozwa na Bw. Kessy Emmanuel Elerai
ambayo kwa sasa inaongozwa na mhandishi Jeremia Mpinga, Kimandolu
inayoongowa na Rayson Ngowi na Themi inayoongozwa na kinabo Meladi
wanachama wa Chadema wengi wao wakiwa ni vijana walilipuka kwa nderemo
na vifijo wakishangilia ushindi huo.