WATU 29 WAHOFIWA KUFARIKI WAKATI WAKICHOTA MAFUTA KWENYE AJALI

Kampala, Uganda. Moto mkubwa umeweka baada ya ajali mbaya ya barabarani kutokea na kuhusisha lori la mafuta. Moto huo umewauwa watu 29 mjini kampala Uganda, hivi punde.

Pia watu wengine 30 wamejeruhiwa vibaya kufuatia tukio hilo.

Maofisa wa polisi wanasema kati ya waliofariki dunia ni raia waliokuwa wanakimbilia kwenye eneo ambako ajali hiyo imetokea kwa ajili ya kuteka mafuta yaliokuwa yakivuja kutoka kwwenye lori hilo.

Maofisa wa serikali wa hivi sasa wako kwenye harakati za kutambua mili ya watu waliofariki dunia kwenye eneo la ajali baada ya watu wengi kuungua vibaya.

Idara ya polisi imesema watu waliofariki dunia waliteketea kiasi cha kutotambulika na itabidi watumie utaalamu wa vinasaba au DNA kutambua miili ya waliokufa.


JIUNGE NA EDMO BLOG SASA

Usipitwe!! Jiunge nasi kupitia Facebook,Twitter na Instagram ili kupata habari zote za town! Usikose kujiunga na Youtube kuangalia video zote kali kutoka Edmo Blog Pekee!, kujiunga bonyeza hapa>>>Youtube

Tupe Maoni Yako lakini Usiandike Matusi



 
© Copyright EDMO BLOG | Designed By Peruzibongo