WASOMI IRINGA WAIPONGEZA RASIMU MPYA YA KATIBA

Baadhi ya wasomi na wananchi mkoani Iringa wamepongeza rasimu ya katiba iliyotangwa jana Jijni  Dar es Salaam na kufafanua kuwa imefuta makosa ya awali yalikuwa kwenye muundo wa Tume ya mabadiriko ya katiba mpya.
 
Akizungumza ofisini kwake mjini hapa Mkuu wa Kitivu cha Sanaa na Sayansi Jamii wa Chuo Kikuu cha Tumain Profesa Seth Nyagava alisema rasimu hiyo inatoa matumaini makubwa kwa Tanzania ijayo kwa kuwa imebabu mbao yote ya msingi yaliyokuwa yakidiwa na wananchi.
 
Alitaja mambo hayo kuwa ni kupunguza madaraka ya rasi,muundo wa muungano kuw ana serikali tatu,kuwa na ukomo wa kipoindi cha ubunge na muundo wa baraz ala mawaziri.
 
Alisema hatua ya mawaziri kuthibitishwa na bunge ni jambo jema kwa kuwa litawezesha wananchi kujenga imani na viongozi wao na kuondoa dhana iliyojengeka kuwa viongozi wanachaguana kwa vigezo vya urafiki.
 
“Mimi sijasoma rasimu yenyewe kwa undani,lakini kwa haya niliyoyasikia nimefurahisha sana nayo,lipo suala la kupungua  kwa madaraka ya rais,muundao wa muungano kuwa na serikali tatu na mawaziri kuthibitishwa na Bunge, masuala haya ni muhimu katia usatwi  na  Ujezni wa Taifa hili,”alisema Profesa Nyagava na kuongeza:
 
“ikiwa mawaziri watathibitishwa na Bunge hali hiyo itaondoa dhana iliyojengeka kuwa  rais aliyoko mdarakani kuchagua watu kwa kutumia vigezo vya urafiki kwa kuwa wahusika watahojiwa kwa kina na kabla ya kuthibitishwa kushika nyazifa zao”.
Profesa Nyagava ambaye alikuwa bado anaipitia rasimu hiyo alisema kazi iliyofanywa na Tume ya mabadiliko ya katiba chini ya Jaji Mstaafu Joseph Warioba inapasw akupongez wana kuongeza kuwa imefuta mawazo na hofu ilikuwa umejengeka wakati wa uundwaji wa baraza kwa madai ya lingeitenda haki.
Kwa upande wake Mhadhiri wa Chuo cha Tumaini ambaye pia ni Mkuu wa Kitivo cha sheria ,Wakili Renatus Mgongo alipongeza tume kuja na rasimu bora inayozingatia haki za bindamu,miiko ya viongozi wa umma,na haki za kupata habari na kusambaza inayotoa uhuru kwa vyombo vya habari kufanya kazi yake.
Alitaja jambo jingine alilodai ni muhumu katika kujenga usatiwa wakitaifa kuw ani kutajwa kwa miiko  ya viongozi wa umma katika rasimu ya katiba hiyo akidai itasaidia kuonyesha dira ya taifa la Tanzania.
“Baada ya kufa kwa zimio la Arusha ambalo lilikuwa na miiko taifa lilibaki bila miiko kwa viongozi wake ,lakini rasimu hii imekuja na majibu ya matakwa ya wananchi kwa kuweka kipengele kinachoelezea utii wa miiko ya viongozi”alisema Mgongo.
Mgongo aliwataka watanzania kuisoma katiba hiyo na kabla ya kuanza kutoa maoni yao ili waweze kuelewa vema rasimu ya katiba hiyo kabla ya kwenda kuijadili.
Kwa Upande wake Mwenyekiti wa Chama cha Wafanyabishara wa Viwanda na wakulima (TCCIA)Tawi  la Iringa Lucas Mwakapungu alisema rasimu ya katiba imejibu madai yaliyomengi ya wanachi.
“Uwepo wa serikali tatu ni hitaji muhumu katrika muundo wa muungano na hii itasaidia hata suala zima la mgawanyo wa madaraka na kurahisha utendaji kazi kwa kila sehemu ya muungano”alisema Mwakapungu


JIUNGE NA EDMO BLOG SASA

Usipitwe!! Jiunge nasi kupitia Facebook,Twitter na Instagram ili kupata habari zote za town! Usikose kujiunga na Youtube kuangalia video zote kali kutoka Edmo Blog Pekee!, kujiunga bonyeza hapa>>>Youtube

Tupe Maoni Yako lakini Usiandike Matusi



 
© Copyright EDMO BLOG | Designed By Peruzibongo