DKT KAWAMBWA NA MULUGO WAMESHINDWA KUONGOZA WIZARA YA ELIMU - SUZAN LYIMO

Kambi rasmi ya Upinzani Bungeni imesema kuporomoka kwa elimu Nchini pamoja na sababu nyingi zilizotajwa na Tume mbalimbali za uchunguzi ni dhahiri kuwa Waziri wa Elimu na Mafunzo ya Ufundi Dkt Shukuru Kawabwa na Naibu wake Philipo Mulugo wameshindwa kuiongoza wizara hiyo hivyo hawana budi kujihudhuru

Kauli hiyo imetolewa na Mh Suzani Lyimo(Pichani) Msemaji Mkuu Kambi rasmi ya Upinzani kwa Wizara ya Elimu na Mafunzo ya Ufundi alipokuwa akisoma hotuba ya Makadirio ya mapato na matumizi kwa mwaka 2013/2014

Katika hotuba yake dakika thelathini Mh Lyimo ameeleza kuwa kutokana na majanga makubwa yaliyotokea katika Sekta ya elimu na kusababisha baadhi ya wanafunzi kupoteza uhai Viongozi hao wataonesha uungwana na uzalendo zaidi kama watawajibika kutokana na hitilafu zilizojitokea.

Akisoma Taarifa ya Kamati ya Kudumu ya Huduma za Jamii kwa niaba ya Mwenyekiti wa kamati hiyo Mh Zabein Mhita yeye anafafanua kuwa upungufu wa walimu hasa maeneo ya Viijjini unasababishwa na Mazingira magumu katika kutekeleza majukumu yao.

Awali akiwasilisha Makadirio ya mapato na matumizi ya fedha waziri mwenye dhamana ya Wizara hiyo Dkt shukuru kawambwa amebainisha yafuatayo.

Wizara hiyo imeomba kutengewa Shilingi Bilioni 689.6 ili kuweza kutekeleza majukumu yake ,kati ya fedha hizo bilioni 330.1 ni kwa ajili ya matumizi mengineyo bilioni 188.1 zimetengwa kwa ajili ya mishahara na bilioni 53.7 zimeobwa kwa ajili ya miradi ya maendeleo.


JIUNGE NA EDMO BLOG SASA

Usipitwe!! Jiunge nasi kupitia Facebook,Twitter na Instagram ili kupata habari zote za town! Usikose kujiunga na Youtube kuangalia video zote kali kutoka Edmo Blog Pekee!, kujiunga bonyeza hapa>>>Youtube

Tupe Maoni Yako lakini Usiandike Matusi



 
© Copyright EDMO BLOG | Designed By Peruzibongo