Watu wawili wilayani Rombo mkoani Kilimanjaro wamefariki dunia kwa kile kinachodaiwa kunywa pombe nyingi kupita kiasi.
Mmoja wa mashuhuda aliyekua na marehemu kabla ya kukumbwa na umauti
alisema kuwa marehemu alikunywa pombe za kienyeji, mbege na pombe
nyingine na baada ya hapo marehemu aliishiwa nguvu.
Tukio hilo lilitokea Mnamo tarehe 28juni mwaka huu katika kata ya Shimbi Tarafa ya Mkuu wilayani hapa.
Wananchi mbalimbali walitoa Maoni yao kuhusiana na matukio hayo huku
wakiwatupia lawama viongozi wa vijiji kwa kushindwa kudhibiti suala la
ulevi hasa uuzaji wa gongo katika kata hiyo ya Shimbi.
Suala la ulevi katika wilaya ya Rombo limezidi kushika kasi licha ya
juhudi mbalimbali zinafonywa na serikali kudhibiti hali hiyo.
Na, Yohane Gervas, Rombo
