JESHI LA POLISI MAKETE LINAMSHIKILIA MWANAFUNZI WA KIDATO CHA TATU KWA TUHUMA ZA KUTOA MIMBA

 Mkuu wa upelelezi(OCCID) wilaya ya Makete Gosbert Komba
========
Jeshi la polisi wilaya ya Makete mkoani Njombe linamshikilia msichana anayesoma kidato cha tatu katika shule ya sekondari Kitulo (jina linahifadhiwa kwa sasa) kwa tuhuma za kutoa mimba ya miezi minne

Akizungumza na ripota wetu Mkuu wa upelelezi wilaya ya makete Bw Gosbert Komba amesema wanamshikilia mwanafunzi huyo baada ya kupatiwa taarifa za kutenda kosa hilo ambalo ni kinyume na sheria za nchi

Amesema wamepata taarifa za msichana huyo kutoa mimba kutoka kwa mwalimu mkuu wa shule hiyo ambapo baada ya mahojiano baina ya polisi na binti huyo, alikiri kutenda kosa hilo

Akizungumzia sakata hilo binti huyo amesema ni kweli ametoa ujauzito huo kwa kutumia vidonge ambavyo hakueleza amevipata wapi ama ameshauriwa na nani kutenda kosa hilo ambapo pia kwa mujibu wa maelezo yake ana kijutia kitendo hicho alichokifanya

“Mimi ni kweli nimetoa mimba na baada ya kufanya hivyo naatamani sana kurudi shuleni kuendelea na masomo, sitaangalia jamii itanielewa vipi ama wanafunzi wenzangu pale shuleni lakini pia zaidi ya yote najutia kitendo nilichokifanya” alisema mwanafunzi huyo wakati akihojiwa na polisi

Amedai kuwa mwanaume aliyempa ujauzito huo amemaliza kidato cha 6 kwa sasa na walianza uhusiano wa kimapenzi tangu januari mwaka huu na alipogundua kuwa amempa mimba mwanafunzi huyo jamaa ametoroka

Kwa mujibu wa jeshi la polisi Makete mwanafunzi huyo anatarajiwa kufikishwa mahakamani kujibu shitaka linalomkabili muda wowote kuanzia sasa, huku Bw. Komba akikiri kuwepo kwa vitendo vya utoaji mimba wilayani hapo ambavyo hufanyika kwa siri kubwa


JIUNGE NA EDMO BLOG SASA

Usipitwe!! Jiunge nasi kupitia Facebook,Twitter na Instagram ili kupata habari zote za town! Usikose kujiunga na Youtube kuangalia video zote kali kutoka Edmo Blog Pekee!, kujiunga bonyeza hapa>>>Youtube

Tupe Maoni Yako lakini Usiandike Matusi



 
© Copyright EDMO BLOG | Designed By Peruzibongo