Bw. Niko Mbwilo akiongea na mwandishi wetu
Edwin Moshi, Makete
Walemavu wilayani Makete wametakiwa kutobweteka na hali ya
ulemavu waliyonayo na badala yake wajishughulishe kufanya kazi mbalimbali
zitakazowafaa kulingana na ulemavu walionao
Kwa kufanya hivyo kutawapunguzia hali ngumu ya maisha waliyonayo
walemavu wengi wilayani hapo kwani kwa kiasi kikubwa ni wategemezi
Hayo yamesemwa na Niko Mbwilo ambaye ni mlemavu
anayejishughulisha na utengenezaji wa bidhaa mbalimbali zinazotokana na miti
aina ya mianzi wakati akifanya mahojiano na mtandao huu
| Niko akiwa kazini |
Mbwilo amesema ulemavu unatofautiana baina ya mtu mmoja na
mwingine, hivyo mtu anatakiwa kuangalia ni kazi gani itakayomuingizia kipato
ambayo anaweza kuifanya badala ya kukaa na kubweteka ama kutegemea misaada
mbalimbali
“Kwa mfano mimi ni mlemavu wa mguu, lakini nikaona ni bora
kubuni shughuli hizi za mikono kwania sina ulemavu wa mikono, hivyo nafanya
kazi kulingana na jinsi nilivyo, hivyo nadhania kila mlemavu akiliangalia hilo
nafikiri maisha yaoa yatakuwa na unafuu”alisema Mbwilo
Amesema ingawa kuna changamoto anazokutana nazo wakati wa
kufanya kazi yake ikiwemo umbali wa kufuata mitia aina ya mianzi anayoitumia
kutengenezea kazi yake, uchakavu wa jingo analofanyia biashara pamoja na ugumu
wa soko lakini hakati tamaa kwa kuwa shughuli hiyo ndiyo inayomuingizia kipato
kwa ajili yake na familia
| Malighafi anayotumia Niko |
Ameongeza kwa kiasi kikubwa bidhaa anazotengeneza huwa
zinategemea wateja wa nje ya wilaya ya Makete kwa kuwa wanaotengeneza bidhaa
kama hizo ni wengi
Baadhi ya bidhaa anazozitengeneza ni nyungo, vikapu, viti,
meza, ambavyo anavitengeneza kwa kutumia mianzi