Mkuu wa wilaya ya Makete Josephine Matiro jumatatu Mei 20 mwaka huu anatarajia kusoma ripoti ya utekelezaji wa shughuli za serikali ndani ya wilaya yake kutoka Januari-Aprili 2013
Kwa mujibu wa taarifa iliyotolewa kwa vyombo vya habari na mkuu huyo, ataisoma taarifa hiyo kwenye ukumbi wa halmashauri ya wilaya ya Makete kuanzia saa tatu na nusu asubuhi, hivyo kuwataka wananchi wote na wadau mbalimbali kufika na kuisikiliza taarifa hiyo