Na Francis Godwin
Mkurugenzi wa Halmashauri ya Manispaa
ya Iringa Bi.Terresia Mahongo (pichani) amesema kuwa ni marufuku
machinga kufanya shughuli zao katika eneo la barabara ya Mashine
tatu ambalo kisheria haliruhusiwi kutumika kwa shughuli hizo.
Kauli ya mkurugenzi Mahongo imekuja
ikiwa ni siku mbili tu zimepita baada ya mbunge wa jimbo la Iringa
mjini mchungaji Peter Msigwa (Chadema) kuwahamasisha machinga
kupitia mkutano wa hadhara kurejea eneo hilo kesho jumapili.
Kwa mujibu wa Mahongo kuwa maamuzi
ya kuwaondoa machinga eneo hilo yalifanyika na baraza la madiwani
hivyo hatua ya machinga hao kurejea eneo hilo ni uvunjaji wa
sheria.