NA FRANCIS GODWIN
Kufuatia shambulio la kulipuliwa kwa kanisa
katoliki la Olasit nje kidogo ya mji wa Arusha na kupelekea watu zaidi
ya 30 kujeruhiwa na mmoja kusadikika kupoteza maisha yake ,askofu wa kanisa la kiinjili la Kilutheri Tanzania (K.K.K.T) Dayosisi ya Iringa Dkt Owdenburg Mdegella
amesema kuwa wanafanya hivyo ni watu ama mtu anayetaka kuvuruga
amani ya Tanzania na kutaka nyumba zote za ibada kuwa na ulinzi .
Askofu Dkt Mdegella ametoa kauli hiyo leo wakati akizungumza katika mahojiaono maalum na mtandao huu kuhusiana na tukio la kulipuliwa kwa kanisa mkoani Arusha.
Kwani alisema
alishapata kukutana na vyombo vya habari kufuatia tukio la kuchomwa
kwa kanisa Zanzibar na tukio la kuuwawa kwa Paroko kwa risasi
huko huko Zanzibar ila ushauri wake alioutoa kwa serikali kuwa
hivi sasa nchi inakundi la watu wanaoendesha ugaidi ,na kutaka
vyombo vya usalama kusaidia kupambana na kundi hilo.
Askofu Dkt Mdegella ametoa kauli hiyo leo wakati akizungumza katika mahojiaono maalum na mtandao huu kuhusiana na tukio la kulipuliwa kwa kanisa mkoani Arusha.
Kwani amesema kuwa hivi sasa amani ya Taifa inazidi kuwa hatarini zaidi kutokana na watu hao wanaoendesha vitendo vya kigaidi kuingia kwa kasi kubwa kushambulia makanisa na kuwa ni vema vyombo vya ulinzi na usalama kusaidia kulinda nyumba za ibada ili kunusuru njama hizo za kigaidi.
Mbali ya kuvitaka vyombo vya usalama kusaidia kulinda makanisa bado alishauri waumini wa makanisa hapa nchi kuwa makini zaidi na ikiwezekana kuongeza ulinzi zaidi katika makanisa yao hasa siku za ibada .
Askofu Dkt Mdegella alisema kuwa yawezekana ni kundi la watu wanaotumia ugaidi kuhatarisha amani ya Tanzania ila pia yawezekana mambo haya ya machafuko yanafanywa na kundi furani la kisiasa kwa lengo la kuichafua serikali ya CCM iliyopo madarakani kama njia ya kuchinganisha umma kuona kama Rais Jakaya Kikwete na chama chake nchi imemshindwa jambo ambalo halipaswi kuungwa mkono na mtanzania yeyeto kwa watu kuchafua amani ili wapate kuingia Ikulu.
Bila kutaja jina la chama cha siasa kinachofanya hivyo wala mtu anayefadhili vitendo hivyo vya kigaidi askofu Dkt Mdegella aliwataka wana siasa na wananchi kuwa kitu kimoja katika kulinda amani ya Taifa hili.
Pia aliulaumu uongozi wa kanisa Katoliki Arusha kwa kushindwa kuimarisha ulinzi kwa siku ya Jana ambapo walitambua wazi wana tukio kubwa na tayari kumekuwepo na vitisho mbali mbali na kuwa iwapo ulinzi ungewekwa eneo hilo yaliyotokea huenda yasingetokea.