ZIFF YAWATAKA WASANII KUPELEKA KAZI ZAO

 
Baadhi ya wasanii wa filamu Bongo, kutoka kushoto ni: JB, Ray, Uwoya, Richie na Wema.
Na Imelda Mtema
TAMASHA la Filamu Zanzibar (ZIFF) limewataka wasanii mbalimbali wa filamu kupeleka filamu zao ili zikaguliwe mapema kuepusha lawama ukifika wakati wa kutoa tuzo.



Akizungumza na Stori 3, mratibu wa tamasha hilo, Hassan Bond ‘Hazt’ amesema wasanii wengi kila mwaka wamekuwa wakitoa lawama kuwa hawakupewa taarifa mapema hivyo mwaka huu wameanza kuwataarifu mapema.

“Tunahitaji kazi zije kwa wingi, tuzikague ili kuzithibitisha kabla tamasha halijaanza kuunguruma miezi kadhaa ijayo,” alisema Hazt.


JIUNGE NA EDMO BLOG SASA

Usipitwe!! Jiunge nasi kupitia Facebook,Twitter na Instagram ili kupata habari zote za town! Usikose kujiunga na Youtube kuangalia video zote kali kutoka Edmo Blog Pekee!, kujiunga bonyeza hapa>>>Youtube

Tupe Maoni Yako lakini Usiandike Matusi



 
© Copyright EDMO BLOG | Designed By Peruzibongo