MUIGIZAJI DAVINA AJIFUNGUA MTOTO WA KIUME

Davina 
Bongo-movie-crew
Muigizaji wa filamu Halima Yahaya ‘Davina’ amejifungua mtoto wa kiume katika Hospitali ya Aga Khan hivi karibuni. 

Msanii huyo mahiri katika tasmia ya filamu nchini Tanzania alikuwa amejawa na furaha wakati alipotembelewa na wa wasanii wenzake kwa ajili ya kumjulia hali na kumpa hongera. 
 
Namshukuru “mwenyezi Mungu kwa kujifungua salama na nimepata Baby boy nimefurahi sana unajua siku mambo ya uzazi yanavyokuwa lakini pia asante kwa nyinyi rafiki zangu kuja kunitembelea na kujua hali yangu na mimi nipo salama kabisa na mtoto yupo sawa,” alisema Davina. Davina alitembelewa na wasanii wenzake katika Hospitali ya Aga khan kumpongeza. 
 
Baadhi ya wasanii hao walioenda kumuona ni Jenifer Kyaka ‘Odama’, Salama Salmin ‘Sandra’, na kiongozi wa kundi la Bongo movie Herith Chumila, wanaonekana pichani chini wakiwa wenye furaha kwa rafiki yao kujifungua salama na kuwaletea mtoto wa kiume.
Source: Pro-24


JIUNGE NA EDMO BLOG SASA

Usipitwe!! Jiunge nasi kupitia Facebook,Twitter na Instagram ili kupata habari zote za town! Usikose kujiunga na Youtube kuangalia video zote kali kutoka Edmo Blog Pekee!, kujiunga bonyeza hapa>>>Youtube

Tupe Maoni Yako lakini Usiandike Matusi



 
© Copyright EDMO BLOG | Designed By Peruzibongo