HATIMAYE filamu mpya ya kimataifa ya Bikira Kidawa imeingia sokoni
kwa kishindo baada ya kuzikimbiza filamu zilizpo mtaani Mtayarishaji wa
filamu na mwandishi wa muswada, Octavian Natalis ‘Mdau Octa’ ameeleza
kuwa, sinema hiyo imeingia sokoni mwishoni mwa wiki iliyopita.
“Filamu ipo sokoni tangu Ijumaa ni wakati wa watazamaji kujionea filamu bora ya Bikira Kidawa,” alisema Octavian.
Akiizungumzia filamu hiyo, alieleza kuwa ni moja ya filamu
zinazoelezea hali halisi ya Mtanzania wa kawaida, ikielimisha kuhusu
ubaya wa mila potofu, mimba za utotoni, wazazi kutengana, malaria na
Ukimwi.
Baadhi ya waigizaji waliotamba ndani ya Bikira Kidawa ni Janet Lameck
aliyeigiza kama kinara, Zubeir Mohamed ‘Niva’, Ruth Suka ‘Mainda’,
Mohamed Fungafunga ‘Jengua’, Korongo Hamis Korongo, Shamila Ndwangila
‘Bi Staa’, Abdallah Mkumbila ‘Muhogo Mchungu’, Fatma Abubakari na
muigizaji aliyetamba na sinema ya Laptop, Hamida Atos pamoja na
waigizaji wengine lukuki.
Filamu hiyo imepigwa picha na kuhaririwa na Suleiman Omar ‘Suleish
Marah’ na kuongozwa naRashid Mrutu aliyewahi kuongoza filamu za
Gongolamboto na Laptop.
Imeandikwa muswada na Octavian Natalis aliyewahi
kuandika filamu za Sanda Nyeusi, Kesi ya Jinai (Babu Seya), Kimya,
Albino Mgeni, Gongolamboto na Laptop. Zaidi ya wasanii 84 wameshiriki
katika kuigiza filamu ya Bikira Kidawa.