CDM/BAVICHA/2013/1.
BARAZA LA VIJANA
CHADEMA (BAVICHA),
CHADEMA WILAYA,
P.O
BOX 599,
KYELA.
25/02/2013
SIMU:0712 725 444
AFISA ELIMU (W) KYELA,
P.O BOX
KYELA.
25/02/2013
Kamati
ya taarifa na ufuatiliaji kyela iliyojumuisha wanazuoni wa kyela na
wajumbe toka katika wilaya ya Kyela iliyoteuliwa na BAVICHA siku ya jumamosi
Tarehe 23/02/2013 chini ya kamati kuu, chini ya chama cha CHADEMA wilaya ya Kyela iliamua kuja kuhoji
na kutoa matamko leo Jumatatu tarehe 25/02/2013 kwa Afisa Elimu Wilaya, kamati
inamtaka Afsa Elimu wa Wilaya kujibu mambo yaliyoainishwa na kuazimiwa na kamati
kuhusu suala la Elimu Kyela kama ifuatavyo;-
1. Afisa
elimu anatathimini vipi kushuka kwa kufaulu kwa wanafunzi? na ni kwasababu zipi
zinapelekea kukithili kwa kufeli kwa wanafunzi hao? Ngazi ya;
v Darasa
la saba
v Kidato
cha pili
v Kidato
cha nne
2. Ni
hatua gani zinachukuliwa na ofisi yako kuthibiti kufeli kuliko kithili kwa
wanafunzi?ni zipi hatua za haraka (immediate solutions) na za muda mrefu (long-term
salutions)?
3. Fedha
za malipo kwa walimu wa muda(part time-form six leaver na wahitimu wa vyuo
vikuu) ,zinalipwa kwa flat rate ya Shilingi ngapi kila mmoja?na ni vigezo vipi
vya malipo vinavyotumika?na Ofisi yako inatenga Shilingi ngapi kwa ajili ya
waalimu hao?
4. Kwanini
baadhi ya shule zinakataa kuwapokea walimu wa mafunzo kwa vitendo(field)kwa
kuzingatia vigezo visivyo na muhimu kwa mfano, eti walimu kutoka UDSM
watasababisha migomo kwa wanafunzi?na Kyela day ikiwa moja ya shule iliyotoa
tamko hilo,ofisi yako ilichukua hatua gani?na inampango gani kwa walimu hawa?
5. Ni
mpango upi mkakati unaotoa mwelekeo wa kuleta umeme mashuleni?ikizingatiwa
shule kama Nkuyu,nguzo zipo karibu kabisa,tatizo ninini?
6. Je
kuto kuwepo kwa vitabu vya kiada(Basic books) mashuleni ni hatua zipi madhubuti
zinazochukuliwa na ofisi yako ili kuleta vitabu hivyo mashuleni?na ni hatua zipi
zinachukuliwa kudhibiti kuenea kwa vitabu vya ziada vinavyotumika kufundishia
mashuleni?
7. Je
wanafunzi waliofeli, ni mpango upi madhubuti ambao Ofisi yako imeweka wa
kuwafanya wanarudi shule,ili kuondoa kundi kubwa la vijana wasio na elimu ya
kutosha kutokana na kufeli kwao?
8. Je
ni utaratibu upi unaotumika kudhibiti masomo ya ziada(tutions) ikizingatiwa
wanoafungua vituo hivyo kwanza hawana sifa katika kufundisha,pili hawanaithibati/mtaala
na ni utaratibu gani unaotumika kufungua vituo hivyo?
9. Maazimio
ya wilaya juu ya uwepo wa mitihani ya Mock kwa kidato cha tatu kama kipimo na
kigezo cha kumfanya mwanafunzi arudi
darasa akifeli,je maazimio hayo yanafuatwa?je upangaji wa fedha za mitihani
hiyo zilijumuisha vitu gani na kwa vigezo vipi?je ni kwa kiasi gani wazazi
wanafahamu juu ya maazimio hayo ?na kama hakuna matokeo tarajiwa(impact) kwa
mitihani hii,kuna umuhimu gani wa uwepo wa mitihani ya mock kwa kidato cha tatu?wito
wa kamati, kama uwepo wa mitihani ya mock ni lazima ni vyema maazimio hayo
yafuatwe na wanafunzi waliokosa alama za maazimio hayo warudie darasa, na kama
haina ulazima ni vyema mitihani hiyo ifutwe na pesa zirudishwe kwa wazazi.
10. Je
kunamitihani mingapi kwa mwanafunzi kutoka darasa moja kwenda darasa lingine,
na inazingatia alama zipi?na je hizo alama zinasimamiwa?
11. Je
ubovu wa maslahi ya walimu likiwa kama sababu moja wapo ya kufeli kwa wanafunzi
kutokana na kushuka kwa morali ya waalimu katika kufundisha,linatathiminiwa
vipi na ofisi yako,na ni njia zipi madhubuti zinachukuliwa ili kutatua tatizo
hili?kwa upande wa vifaa duni vya kufundushia kama nyenzo anazotumia mwalimu,je
ofisi yako imechukua hatua gani kuhakikisha walimu hawa wanapata vifaa
bora?hasa vitabu na vifaa vya maabara.
12. Umbali
wa baadhi ya shule kutoka majumbani,unadhibitiwaje hasa kwa shule za vijiji vya
mbali na Kyela mjini,kwa mfano wanafunzi wanaotoka kijiji cha Itekenya kwenda
katumba songwe sekondari ni urefu mkubwa mno,ipo mikakati ipi katika kujenga
mabweni ili kuepusha mazingira hatarishi?
13. Uchaguzi
wa wanafunzi kutoka darasa la saba kwenda kidato cha kwanza alama zimeshushwa
kutoka 250 miaka michache iliyo pita kwenda 70 kwasasa,je ofisi elimu wilaya
haioni kuwa hiki ni moja ya kigezo cha kutengeneza wanafunzi watakao feli na
kuhitimu na sifuri na si kufaulu? je kuhamisha darasa kutoka shule ya msingi na
kwenda shule ya sekondari kwa mfano kutoka Nkuyu shule ya msingi kwenda Nkuyu
sekondari au kutoka mbogela shule ya msingi kwenda Kyela sekondari,ofisi yako
haioni kwamba inazorotesha elimu kwa kutengeneza darasa lilelile,lenye
wanafunzi walewale wa alama zilezile na kufeli zaidi?
14. Kwanini
shule ya kyela sekondari inawafukuza na kuto wapa ruhusa wanafunzi wa shule
nyingine za sekondari katika kutumia miundombinu hiyo ikiwamo umeme wakati wa
masomo ya ziada jioni?je ofisi yako imechukua hatua gani katika kuwafanya
wanafunzi hawa wapate fursa sawa za kutumia umeme huo?wanafunzi wa kyela sekondari,
achilia mbali shule nyingine za sekondari hawawezi kusoma zaidi ya saa kumi na
mbili jioni,je hili sio tatizo linaloongeza kufeli?kwa uhakika upi wanafunzi
hawa wanaweza kujisomea wakiwa majumbani?
HITIMISHO
kutokana
na matamko hayo(orders) ya mambo ya hapo juu kamati teule na huru ya BAVICHA na
iliyojumuisha wanazuoni na wajumbe wengine inatoa siku mbili kuanzia jumatatu
ya tarehe 25/02/2013 ifikapo jumatano ya tarehe 27/02/2013 asubuhi umma uwe
umepata majibu ya kina kutoka kwa Afisa Elimu wa wilaya ya kyela na yanayokidhi
(ambayo ni relevant)yenye ukweli,utashi na ubora kuhusiana na suala la elimu.Majibu
ya Afisa Elimu wa Wilaya yapitie aidha vyombo vya habari au ofisi ya kamati
teule ya BAVICHA chini ya ofisi kuu
chadema wilaya.kinyume na maagizo hayo NGUVU
YA UMMA itatumika.
NAKALA;
MKUU WA WILAYA-KYELA.
MKURUGENZI WILAYA –KYELA.
M/KITI WA HALMASHAURI-KYELA.
CHADEMA WILAYA-KYELA.
CHADEMA BAVICHA-KYELA.
____________________________ ______________________
M/KITI
KAMATI YA UFUATILIAJI, KATIBU
BAVICHA(W),
LUSAJO
BERNARD MWAMAFUPA, NSAJIGWA BONIFACE
0712
725 444/0687 725 444. 0762 011 709/0658 290
813.
