VYOMBO VYA HABARI VYA UMMA VIACHWE HURU - WADAU



Vyombo vya habari vya uma hapa nchini, vimetakiwa kuachwa vifanye kazi yake vyenyewe bila kuingiliwa na mtu yoyote kwa kuwa vina haki ya kutoingiliwa katika utendaji wake wa kazi

Wakizungumza na mtandao huu katika maadhimisho ya siku ya redio duniani wakazi wa jiji la Dar es Salaam, wakazi hao wamesema vyombo vingi vya uma hapa nchini vimekuwa vikiingiliwa katika utendaji kazi hali inayosababisha uonevu kwa wengine

Kwa upande wake mwandishi mkongwe wa habari hapa nchini Ndimara Tegambagwe amesema vyombo hivyo havitakiwi kuingiliwa na serikali, waziri, mbunge, ama kiongozi yeyote kwani kunasababisha habari za watu wengine kutosikika

“Wakati wa uchaguzi vyombo hivyo mara nyingi unaona vinapendelea serikali sasa hili si nzuru, kwani vinaendeshwa kwa kodi ambazo tunalipa watanzania wote hata wale ambao habari zao hazitangazwi kwenye vyombo hivyo”alisema Tegambagwe

Naye Pili Mtambalike kutoka (MCT) amesema vyombo vya habari vya uma ni mali ya uma hivyo vinatakiwa kutangaza habari zote bila kukatazwa na mtu yoyote tofauti na sasa ambapo inaonekana vingi vinapendelea serikali

“Hakuna haja ya kupendelea vyombo hivi vinatakiwa kutangaza habari zote kwa usawa na si kupendelea zaidi za mwajiri ambaye ni serikali sasa hapa uhuru haupo” alisema Bi. Mtambalike

Leo ni maadhimisho ya siku ya redio duniani ambapo mataifa yote duniani yanaadhimisha siku hiyo


JIUNGE NA EDMO BLOG SASA

Usipitwe!! Jiunge nasi kupitia Facebook,Twitter na Instagram ili kupata habari zote za town! Usikose kujiunga na Youtube kuangalia video zote kali kutoka Edmo Blog Pekee!, kujiunga bonyeza hapa>>>Youtube

Tupe Maoni Yako lakini Usiandike Matusi



 
© Copyright EDMO BLOG | Designed By Peruzibongo