Hii
ndio ajali iliyosababisha vifo vya familia hizo. Na picha za juu ni Rais
Jakaya Mrisho Kikwete akifariji ndugu, jamaa na marafiki wa familia
zilizoondokewa na watoto na wazazi kufuatia ajali ya barabarani maeneo
ya kijiji cha Kibiki, Ubena Zomozi katika mkoa wa Pwani Februari 11,
2013 iliyoua hapohapo watu wanane wakiwemo wanafunzi wa Shule ya
Sekondari ya Chalinze baada ya gari dogo aina ya Toyota Mark II
lililokuwa limebeba abiria wanane kugongana uso kwa uso na lori. (Picha
na Ikulu)
RAIS Jakaya Mrisho Kikwete Februari 16, 2015
amekwenda kuhani na kufariji ndugu, jamaa na
marafiki wa familia
zilizoondokewa na watoto na wazazi kufuatia ajali ya barabarani maeneo
ya Kijiji cha Kibiki, Ubena Zomozi mkoani Pwani iliyotokea Februari 11,
2013 na kupoteza
hapohapo maisha ya watu tisa wakiwemo wanafunzi wa
Shule ya Sekondari ya Chalinze-
baada ya gari dogo aina ya Toyota Mark II
lililokuwa limebeba abiria wanane kugongana uso
kwa uso na roli la
mizigo.
Familia alizokwenda kuhani na kuzifariji ni pamoja na za marehemu
Hassan Erasto Kurunge (57),
Maria Sadiki (52) na mtoto wa mwaka mmoja
Samweli Ismail wa kata ya Ubena. Wengie ni
marehemu Essau Enos Mwamgingo
(16), Stella Isaack Kazimoto (18), Bahati George Mbena (17)
na Latifa
Maneno (17)
Akiwa ameongozana na Mkuu wa Mkoa wa Pwani, Mwantumu Mahiza na Mkuu
wa Wilaya
ya Bagamoyo, Ahmed Kipozi, Rais Kikwete alieleza kusikitishwa
kwake kwa ajali hiyo, na
kuwataka madereva wawe makini katika kuzingatia
sheria za usalama barabarani
Rais Kikwete alisikitishwa zaidi kwa taarifa kwamba gari hilo dogo
lilikuwa limebeba abiria
wanane, na kuwa dereva wake ambaye pia
alipoteza maisha, hakuwa makini katika kuzingatia
sheria za usalama
barabarani.