ZAIDI YA WANAFUNZI 600 SM KISEGESE RUNGWE WANAJISAIDIA VACHAKANI

Na Ibrahim Yassin Rungwe,

ZAIDI ya wanafunzi 600 wa shule ya msingi Kisegese wilayani  Rungwe  mkoani  Mbeya  wapo hatarini kupata  magonjwa  ya  milipuko  kutoakana  na  kukosa  huduma  ya  vyoo  ali  inayowalazimu  wanafunzi  hao  kujisaidia  katika  vichaka  vilivyopo  pembezoni  mwa shule  hiyo, 

Ali hiyo iligunguliwa   siku  za  hivi  jana  na mwandishi wa gazeti  hili  alipofanya  ziara  ya  kushtukiza  katika  harmashauri  mpya  ya  busokelo  ambapo  wananchi  wa  kata  ya  kisegese walitoa  kero hizo  kuwa  shule  yao  imetelekezwa  na  serikali,

Wakizungumza  kwa  nyakati  tofauti  wananchi hao  walidai kuwa  shule  yao  mbali na  wao  kuchangia nguvu  kazi  katika ujenzi  wa  kuiendeleza  shule  hiyo lakini Halmashauri  kupitia  idara ya elimu wameshindwa  wameshindwa  kuchangia  nguvu kazi  hizo na kuona kuwa  serikali imewatenga,

Wanannchi  hao  wakiongozwa  na  John Mwaisumo  walizitaja  changamoto  zinazoikabili shule  hiyo  kuwa  ni  ukosefu  wa matundu ya vyoo,ofisi  ya  waalimu na vifaa vya ofisi, vyumba vya madarasa,madawati  na  upungufu  wa  waalimu inayopelekea wanafunzi   kushuka  kitaaluma,

Mkuu  wa shule  hiyo Mwl  Patric Nyimbo alikiri  kuwepo  na changamoto hizo  katika  shule yake  na  kudai  kuwa,ni kwali  shule hiyo  ina kabiliwa  na changamoto  hizo kwa  muda mrefu,shule  hiyo  inahitaji kupatiwa  waalimu haraka kwani  waalimu  waliopo ni wanne tu ukilinganisha na idadi kubwa ya wanafunzi  ambao  wamezidi  600,

Mwl  Nyimbo alitaja mahitaji  mengine  kuwa  ni  matundu  10 ya  vyoo yaliyopo ni manne,ofisi ya waalimu,meza na kabati,ambapo kwasasa  ofisi ya  waalimu  wa  shule  hiyo imejengwa  kwa  mianzi na  kukosa  thamani  za ndani,

Mwenyekiti  wa kijiji  cha  Kisegese Nasubile  Mwasiku naye kwa  upande  wake  aliishutumu  halmashauri  ya wilaya  hiyo kuwa imeshindwa  kuunga mkono jitihada  za wananchi  kuchangia maendeleo ya shule hiyo,na kuwa wananchi  walijenga jingo  la  madarasa  mawili kwa  mtambao  wa  panya  ambalo limekaa zaidi  ya  miaka  nane halmashauri imeshindwa  kulipaua kitu ambacho kinawakatisha tama wananchi  kuchangia  maemdeleo,

Diwani  wa  kata  hiyo Edson  Mbila alikiri kuwepo  na  changamoto  hizo  na  kudai  kuwa  tayari amezipeleka  kwa  afisa  elimu msingi  wa  wilaya ambaye  waliongozana  kwenda  kupeleka  tatizo  hilo kwa  mkurugenzi  na kinacho  subiriwa  sasa  ni  utekelezaji wa  kuondoa  tatizo  hilo,

Mkurugenzi  wa  halmashauri  mpya  ya  Busokelo  wilayani  hapa Imelda Isuza, alikiri  kupokea  tatizo  hilo na kwamba tayari  wametega  fedha  mil 10 katika  bajeti  ya  mwaka 2012-2013 kwa  lengo  la kuondoa  changamoto  hizo,ambalo  linawakatisha  tama wananchi  kuchangia  nguvu  kazi katika kujiletea maendeleo  ya  kata  hiyo.


JIUNGE NA EDMO BLOG SASA

Usipitwe!! Jiunge nasi kupitia Facebook,Twitter na Instagram ili kupata habari zote za town! Usikose kujiunga na Youtube kuangalia video zote kali kutoka Edmo Blog Pekee!, kujiunga bonyeza hapa>>>Youtube

Tupe Maoni Yako lakini Usiandike Matusi



 
© Copyright EDMO BLOG | Designed By Peruzibongo