Na Fransis Godwin
WAKATI
mbunge wa jimbo la Iringa mjini mchungaji Peter Msigwa (pichani )na viongozi wa chama cha Demokrasia
na maendeleo (Chadema) leo walijitolea kufanya usafi katika eneo la
kitanzani mjini Iringa kama njia ya kuhamasisha usafi, wapiga kura wa
jimbo hilo wameonyesha kutofautiana na uamuzi huo wa mbunge kufanya
usafi huku baadhi yao wakidai kuwa jimbo hilo limemsinda kuongoza na
ndio sababu ya uchafu kuzagaa kila kona ya mji .
"
Mbunge wetu leo anajitolea kufanya usafi siku zote alikuwa wapi
hadi uchafu unazangaa kiasi hiki mitaani .....tunamtaka Msigwa kufanya
kazi kama wabunge wengine na kuachana na siasa za kuunga unga na
kutafuta umaarufu kwa watu "
Wakizungumza l;eo kwa nyakati tofauti wananchi wa jimbo la Iringa mjini
walisema kuwa mji wa Iringa umeendelea
kuzidiwa na uchafu na kuwa mbali ya mbunge kujitolea kufanya usafi
pamoja na wanachama wa Chadema ila bado hatua hiyo haiwezi kutatua
tatizo la uchafu na badala yake uchafu wa Manispaa ya Iringa
utaendelea kuwepo .
Juma
Husein mkazi wa Kitanzini katika Manispaa ya Iringa alisema kuwa
mbunge wao anatafuta umaarufu wa kisiasa na kusahau kuwa yeye ni
mbunge wa jimbo la Iringa mjini na mwakilishi wa wananchi hao
bungeni hivyo alipaswa kutafuta ufumbuzi wa kudumu wa uchafu katika
jimbo lake badala ya kufanya
usafi kwa misingi ya kisiasa huku akitambua kufanya hivyo ni
kujichongea mwenyewe kwa wananchi kuwa kumbe ameonyesha kushindwa
kuongoza jimbo hilo na ndio sababu ya taka kuzagaa kila kona.
Husein
alisema ni vema mbunge Msigwa kwenda kujifunza katika jimbo la
Moshi mjini ambalo pia linaongozwa na mbunge wa Chadema na kuona kama
mbunge huyo ametumia mbinu kama hiyo kusafisha mji ama kuna mbinu
nyingine inatumika badala ya hiyo ya zima moto inayotumiwa na mbunge
Msigwa sasa ya kukodi magari ya
usafi.
Aidha
alisema kuwa kwa kuwa Manispaa ya Iringa inakabiliwa na tatizo la
magari ya kusomba takataka na uhaba wa vyombo vya kuhifadhia takataka
mbunge Msigwa kwa kutumia mfuko wa jimbo alipaswa kuanza
kushughulikia kero hiyo badala ya kukodi magari kwa siku moja ili
kutaka kuonekana kuwa ni mchapakazi wakati siku zote yupo mjini
Iringa na uchafu huo upo.
Kwa
upande wake mbunge Msigwa alipoulizwa na mwandishi wa habari hizi
kuhusiana na utaratibu huo alisema kuwa kazi ya mfuko wa jimbo
si kwa ajili ya kusafisha mji na kuwa yeye ataendelea kusafisha mji
kwa muda wa siku mbili hizi kabla ya kwenda bungeni .
Msigwa
alisema kuwa kupitia ofisi yake tayari amekwisha changisha
kiasi cha shilingi milioni 16 kwa ajili ya kununua gari ya kubeba
taka katika Manispaa ya Iringa ili kupunguza tatizo la uchafu katika
mji huo.
Afisa
afya wa Manispaa ya Iringa Severin Tarimo alipotafutwa na
mwandishi wa habari hizi ili kueleza mikakati ya Manispaa ya Iringa
juu ya hali ya uchafu inayoendelea kuukumba mji huo alidai kuwa
kwa sasa yupo likizo hivyo anayeweza kujibia hilo ni yule
aliyemwachia ofisi.
"Nazungumza na nani ....sasa mimi nipo likizo bwana naomba uongee na mtu mwingine" alikata simu
