wanahabari mkoa wa Iringa wakiwa katika ofisi ya klabu ya
waandishi wa habari mkoa wa Iringa (IPC) leo wakati wa kikao chao cha
kuelezea lengo la kufanyika kwa mkutano wa wadau wa habari siku ya
jumamosi wiki hii pamoja na kuzindua rasmi IPC VICOBA ili kuwasaidia
wanachama wake kukopa fedha za maendeleo
katibu mtendaji wa IPC Frank Leonard akionesha katiba ya IPC VICOBA ambayo itazinduliwa rasmi siku ya jumamosi wiki hii
Na Francis Godwin
Klabu ya wanahabari mkoa wa Iringa (IPC) inataraji kufanya mkutano
mkubwa wa wadau wa habari mkoa wa Iringa ikiwa ni pamoja na
kuzindua rasmi asasi ya mikopo ya IPC VICOBA itakayowawezasha
wanahabari mkoani Iringa kukopa fedha za kuanzisha miradi ya
kimaendeleo ya kujenga nyumba pamoja na kununua vifaa vya kazi.
Katibu mtendaji wa IPC Frank Leonard akizungumza na wanahabari leo katika ofisi ya IPC amesema kuwa lengo la mkutano huo ni kupokea changamoto mbali mbali za wadau juu wa wanahabari mkoa wa Iringa pamoja na kuzindua rasmi taasisi hiyo ya mikopo kwa wanahabari ya IPC VICOBA .
Hivyo alisema katika mkutano huo wa wadau ambao pia utatanguliwa na mdahalo uliaandaliwa na asasi za kiraia ya ISICO mkoa wa Iringa kwa ajili ya kujadili suala zima la mabadiliko tabia nchi utafanyika kwenye ukumbi wa Hinglands mjini Iringa.
Hivyo amewataka wanahabari mkoa wa Iringa na wadau wa habari kujitokeza kwa wingi katika mkutano na mdahalo huo ambapo mdahalo utaanza mida ya saa 5 asubuhi na kumalizika muda wa saa 8 mchana na baada ya hapo katika ukumbi huo utaendelea mkutano huo wa wadau wa vyombo vya habari pamoja na uzinduzi wa IPC VICOBA .
Leonard amesema kuwa viongozi mbali mbali wa vyama vya siasa na serikali wamealikwa katika siku hiyo kufika kwenye mkutano huo wa wadau wa habari.
Katibu mtendaji wa IPC Frank Leonard akizungumza na wanahabari leo katika ofisi ya IPC amesema kuwa lengo la mkutano huo ni kupokea changamoto mbali mbali za wadau juu wa wanahabari mkoa wa Iringa pamoja na kuzindua rasmi taasisi hiyo ya mikopo kwa wanahabari ya IPC VICOBA .
Hivyo alisema katika mkutano huo wa wadau ambao pia utatanguliwa na mdahalo uliaandaliwa na asasi za kiraia ya ISICO mkoa wa Iringa kwa ajili ya kujadili suala zima la mabadiliko tabia nchi utafanyika kwenye ukumbi wa Hinglands mjini Iringa.
Hivyo amewataka wanahabari mkoa wa Iringa na wadau wa habari kujitokeza kwa wingi katika mkutano na mdahalo huo ambapo mdahalo utaanza mida ya saa 5 asubuhi na kumalizika muda wa saa 8 mchana na baada ya hapo katika ukumbi huo utaendelea mkutano huo wa wadau wa vyombo vya habari pamoja na uzinduzi wa IPC VICOBA .
Leonard amesema kuwa viongozi mbali mbali wa vyama vya siasa na serikali wamealikwa katika siku hiyo kufika kwenye mkutano huo wa wadau wa habari.