| Mkurugenzi wa Manispaa ya Iringa, Theresia Mahongo |
Na Frank Leonard ,Iringa
HALMASHAURI
ya Manispaa ya Iringa imependekeza viwango viwili tofauti vitakavyotumika
kukodi mtambo wake wa kuchonga barabara (greda).
Mtambo huo ulinunuliwa hivi karibuni kwa zaidi ya Sh Milioni
581 zilizokopwa kutoka benki ya CRDB.
Mkurugenzi
wa Halmashauri ya Manispaa ya Iringa, Theresia Mahongo alisema kwa wateja wa nje
watakodi mtambo huo kwa Sh 800,000 kwa saa kumi.
“Na
iwapo kata au mamlaka ya serikali itahitaji kulitumia gharama itakuwa Shilingi
250,00 kwa saa kumi,” alisema.
Pamoja
na gharama hizo, Mahongo alisema wateja watalazimika pia kugharamia mafuta na
dereva.
Aliyasema
hayo kwenye kikao cha makadirio ya mapato na matumizi kwa mwaka 2013/2014 na
mapitio ya bajeti ya mwaka 2011/2012 na Julai hadi Desemba, 2012.
Akiwasilisha
mapendekezo ya mapato na matumizi ya halmashauri kwa mwaka 2013/2014, Mahongo
alisema wanakadiria kukusanya zaidi ya Sh Bilioni 23.3 kutokana na vianzoa
mbalimbali.
Alisema
kati ya mapato hayo zaidi ya Sh Bilioni 20.2 ni ruzuku kutoka serikali kuu na
Sh Bilioni 3.1 kutoka vyanzo vya halmashauri.
Wakati
huo huo, kikao hicho kilipokea maoni yaliyotolewa na kamati mbalimbali za
kudumu za halmashauri hiyo.
Baadhi
ya maoni hayo ni pamoja na kuboresha masoko ya Kihesa na Mashine Tatu ili
yasadie kuongeza mapato ya halmashauri.