MKUU
wa
Wilaya ya Hanang’ Mkoa wa Manyara Christina Mndeme amepiga marufuku
mila
potofu inayoendelea wilayani hapo ya kuwakeketa wasichana na
atawachukulia hatua kali za kisheria wanaofanya kitendo hicho
Taarifa
hiyo
ameitoa wakati akiongea na waandishi wa habari wilayani hapo
mkoani Manyara.
Alisema
kuwa
tabia ya baadhi ya watu wa jamii ya wabarbaig na wairaq kuendelea
kuwakeketa watoto wao wa kike kwa njia ya siri inatakiwa kukomeshwa mara
moja
kabla hajachukua hatua.
Pia
alibainisha kuwa japokuwa tabia hiyo imepungua
kwa kiasi fulani wilayani humo lakini bado inaendelea kwa baadhi yao
kuwafanyia
mila hiyo potofu kwa kuwakeketa watoto wao wa kike kwa njia ya siri.
Aliendelea
kusema kuwa madhara ya kuwakeketa wasichana ni makubwa
kwani wanapata maumivu makali wakati wa kufanyiwa vitendo hivyo vya
kikatili na
pia wanaweza kuambukizwa maradhi pindi wakikeketwa.
Amewataka
wakazi
hao wabadilike kwa kuachana na mila potofu zilizopitwa na wakati kwani
hivi sasa watu wengi wameshatambua kuwa kitendo hicho ni jambo la
kikatili
hivyo halipaswi kufanyika kama miaka iliyopita
“Pamoja
na
matatizo hayo pia wakati wa kujifungua mama mjamzito anapata shida sana
kutokana na kufanyiwa kitendo hicho hivyo jamii iache tabia hiyo mara
moja
kwani mila hiyo ni potofu na imepitwa na wakati,” alisema Mndeme.
Nao
baadhi
ya wakazi wa wilaya hiyo wameeleza kuwa hivi sasa
vitendo vya ukeketaji vinafanyika kwa njia ya siri,baada ya jamii ya
wairaq na
wabarbaig ambao ni wengi wilaya humo kubaini kwamba Serikali haipendi
jambo
hilo kufanyika.
“Watu
wanaogopa
Serikali na wanafanya vitendo hivyo kwa njia ya siri,kwa kuogopa
kuwekwa ndani ila baadhi yao wanawakeketa wakiwa wadogo wengine wanagusa
tu
hilo eneo na wengine wanawapaka ugoro,” walisisitiza.
Walimalizia kwa kusema kuwa baadhi ya watu wa vijiji vya
Masqaroda,Gunyoda,Simbay,Getamuhog Gissambalang,Gidahababieg na
Endasaboghechan
vya wilayani hiyo,hadi hivi sasa bado wanaendelea na vitendo hivyo vya
kukeketa
wasichana.
