SOKO KUBWA LA MAHINDI KUJENGWA KATA YA ENGUSERO



Soko kubwa la mahindi linatarajiwa kujengwa  kwenye kata ya Engusero wilayani Kiteto ili kuwanufaisha wakulima wake na kuwawezesha wauze mazao yao karibu pindi wakiyavuna mashamabani.
Taarifa hiyo imetolewa  na Mkuu wa wilaya hiyo Martha Umbulla,wakati akiongea na vyombo vya habari  kuhusiana na mafanikio ya Serikali ya awamu ya nne na utekelezaji wa ilani ya CCM,mwaka 2005 hadi Desemba 2012.
Pia alisema kuwa  lengo la kujenga soko hilo kwenye kata ya Engusero ni kuhakikisha wakulima wanainufaisha wilaya hiyo kwani hivi sasa wanauza mazao yao kwenye soko la Kibaigwa wilaya ya Kongwa mkoani Dodoma.
Aliongeza kuwa  mwaka jana walifanikiwa kuzalisha zaidi ya tani 120,000 za mahindi hivyo watatumia fursa hiyo kwa kujenga soko lao eneo la Engusero kwani robo tatu ya mahindi yanayouzwa kwenye soko la Kibaigwa yanatokea Kiteto.
Aidha aliendelea kusema kuwa  asilimia 80 ya wakulima wa wilaya ya Kiteto wanajishughulisha na kilimo cha mahindi na pato la wilaya hiyo linategemea kuchangiwa kupitia mazao ya kilimo kwa asilimia 38 na wakulima 156,199 wamepatiwa mafunzo.
Mkuu wa wilaya hiyo ameeleza kuwa wa upande wa kilimo cha umwagiliaji wameandaa skimu za umwagiliaji kwenye vijiji vya Sunya,Olgila na Ngipa ambapo wakulima wake wanajihusisha na kilimo cha mahindi na mbogamboga.  
 ‘’Waandishi wa habari pamoja na hayo tumepiga hatua kubwa kwenye suala la kilimo kwani tumetenga kilomita za mraba 3,800 kwa ajili ya kilimo cha mazao mbalimbali ikiwemo mahindi,alizeti,mbaazi na mtama mweupe,” alisema Umbulla.
Aliongeza kuwa  kupitia vikundi vya kuweka na kukopa (Saccos),benki za jamii vijijini (Vicoba) na vyama vya ushirika (Amcos) wana vikundi hao hutumia hisa zao kwa kununua mazao na kuyahifadhi ghalani na  kuyauza pindi bei ya mazao ikipanda.
Alisema kuwa hivi sasa wakulima wengi wa wilaya ya Kiteto wamepiga hatua kubwa katika uhifadhi wa mazao ghalani ili waendeshe shughuli za maisha wakati wa kusubiri bei ya mazao ipande ndipo waweze kuiuza.
 


JIUNGE NA EDMO BLOG SASA

Usipitwe!! Jiunge nasi kupitia Facebook,Twitter na Instagram ili kupata habari zote za town! Usikose kujiunga na Youtube kuangalia video zote kali kutoka Edmo Blog Pekee!, kujiunga bonyeza hapa>>>Youtube

Tupe Maoni Yako lakini Usiandike Matusi



 
© Copyright EDMO BLOG | Designed By Peruzibongo