MWANDISHI
wa kujitegemea mkoani Arusha anayeandikia vyombo mbalimbali ikiwemo
Zanazibar leo,Dira, redio sunrise pamoja na magazeti ya udaku , Joseph
Ngilisho maarufu kama “”Jb’” leo 29 jan 2013 amefikishwa mahakamani kwa
makosa matatu ya kuomba, kushawishi na kupokea Sh. 500,000 ikiwa ni
sehemu ya rushwa ya Sh. Milioni 2 alizoomba.
Mbele ya Hakimu
Mkazi wa Mahakama ya Arusha, Hawa Mguruta, Mwendesha Mashtaka kutoka
Taasisi ya Kupambana na Kuzuia Rushwa (Takukuru), Rehema Mteta, alidai
kuwa Ngilisho alifanya makosa hayo kwa siku na nyakati tofauti jijini
hapa.
Katika shtaka la
kwanza, Rehema alidai kuwa mnamo Januari 12, mwaka huu, aliomba rushwa
ya Sh. Milioni 2 kutoka kwa Phil Makini Kleruu ambaye ni ofisa
mwandamizi wa Jumuiya ya Afrika Mashariki, ili asimwandike vibaya
kwenye gazeti la Dira.
Alidai katika shtaka
la pili, Januari 25 mwaka huu, Ngilisho aliomba hongo kutoka kwa Kleruu
ili amsafishe kwenye gazeti hilo baada ya kumwandika.
Alitaja shtaka la
tatu kuwa Januari 28, mwaka huu, Ngilisho alikamatwa akiwa amepokea Sh.
500,000 ikiwa ni sehemu ya Sh. Milioni 2 alizokuwa ameomba.
Hata hivyo, Ngilisho ambaye anatetewa na wakili Edmund Ngelemi, alikataa kufanya makosa hayo mbele ya mahakama hiyo.
Hakimu Mguruta
aliaahirisha kesi hiyo hadi Februari 12, mwaka huu itakapotajwa tena na
akamruhusu kudhaminiwa na watu watatu, mmoja wao akiwa ni mtumishi wa
umma.
Wakati wadhamini hao
wakiwasilisha nyaraka zao za kumdhamini, Hakimu Mguruta alizikataa
baada ya kuona zilikuwa zina hitilafu na aliwataka warudi na kupata
barua zingine zilizokuwa zimekamilika na hali hiyo ilimfanya Ngilisho
kwenda mahabusu hadi pale dhamana yake itakaposhughulikiwa.
Nje ya mahakama hiyo
baadhi ya ndugu,jamaa na marafiki wakiwemo waandishi wa habari mkoani
hapa walishikwa na butwaa mara baada ya mwandishi huyo kutinga
mahakamani hapo huku akificha sura yake kwa kuhifia kupigwa picha.
SOURCE:BLOG YA JAMII
JIUNGE NA EDMO BLOG SASA
Usipitwe!! Jiunge nasi kupitia Facebook,Twitter na Instagram ili kupata habari zote za town! Usikose kujiunga na Youtube kuangalia video zote kali kutoka Edmo Blog Pekee!, kujiunga bonyeza hapa>>>Youtube
Tupe Maoni Yako lakini Usiandike Matusi