| Baadhi ya madiwani wakiwa katika kikao cha baraza maalum la kupokea na kujadili na kupitisha rasimu ya mpango bajeti ya halmashauri hiyo. (picha zote na Denis Mlowe) |
| Mkurugenzi wa halmashauri ya Wilaya ya Iringa akizungumza na baraza la madiwani hawako pichani. |
Mwenyekiti wa halmashauri ya Wilaya ya Iringa Steven Mhapa akizungumza na baraza la madiwani katika kikao maalumu cha madiwani
Na Denis Mlowe – Iringa
Kiasi cha shilingi milioni 215 kutumika katika ujenzi wa
madarasa, nyumba za walimu na vyoo katika Halmashauri ya Wilaya ya Iringa Vijijini.
Hayo yamesemwa na Afisa Elimu wa Halmashauri ya Wilaya ya
Iringa Seleman Pandawe wakati akizungumza mbele ya baraza la madiwani katika
kikao maalum cha kamati ya fedha, mipango na utawala na baraza la madiwani kwa
lengo la kupokea na kujadili na kupitisha rasimu ya mpango bajeti ya
halmashauri ya Wilaya kwa mwaka 2013/ 2014 kikao kilichofanyika katika Ukumbi
wa Siasa ni Kilimo.
Alisema kwamba Ujenzi huo utaokaokamilika mwezi Juni mwaka
2014 utazinufaisha shule za zilizoko katika Wilaya hiyo na fedha hizo
zimetokana na mapato ya ndani na nyingine kutoka Serikalini kwa mpango wa fedha
wa bajeti ya 2013/ 2014.
Pandawe alizitaja shule 20 ambazo zitanufaika na ujenzi wa
madarasa ni shule za Ng’enza, Idodi, Ilolo Mpya, Ikengeza, Kinyika,Mkombe,Mfyome,
Chamgogo, Matalawena na Makadufu aidha aliongeza kusema shulre nyingine ni
Ukombozi, Mwanyengo, Kidilo,Kiwewe, Makuka, Lumuli, Mkomilenga, Sasamambo na
Nyakavangala.
Nyumba za walimu zitajengwa katika shule za Kidilo,
Ukombozi, Makadupa, Nyamihuu, Mlanda,Mbuyuni,Kalenga, Kihanga, Kinyali na
Kitanewa na ujenzi wa vyoo vya vyenye matundu 50 utazinufaisha shule za Ihomba itakayopata
matundu 30 na shule ya Kinywang’anga watapata matundu 20.