SERIKALI WILAYANI MAKETE YAWAKUNA WANANCHI

Mtangazaji wa Kitulo Fm Aldo Sanga (kulia) akimhoji mwenyekiti wa CCM wilaya ya Makete Francis Chaula

Mwenyekiti wa umoja wa makanisa wilaya ya Makete Padri Haule akizungumza na mtandao huu

katibu wa CCM wilaya ya Makete Bw. Miraji Mtaturu

Mtangazaji wa Kyela Fm na mwandishi wa gazeti la majira bw. Israel Mwaisaka

Serikali imepongezwa kwa kuanzisha utaratibu wa kutoa taarifa ya mafaniko ya serikali kwa wananchi wake kila baada ya miezi minne na kusema kuwa utaratibu huo utasaidia wananchi kuwa na imani na serikali yao

Wakizungumza na wanahabari mara baada ya Mkuu wa wilaya ya Makete Josephine Matiro kusoma taarifa ya mafanikio ya serikali ya awamu ya nne tangu 2005-2012, wadau hao wamesema hali hiyo itasaidia hata wao kutoa maoni yao kuhusu serikali pale itakapoonekana mambo hayaendi sawasawa

Kwa upande wake Mwenyekiti wa CCM wilaya ya Makete Bw. Francis Chaula amesema wao kama chama wanaupongeza utaratibu huo kwa kuwa ni mzuri na unaweka wazi shughuli zinazofanywa na serikali na wali ilipofikia

“Unajua sasa hivi ni rahisi kuishauri serikali pale itakapotoa taarifa na kuelewa wapi tulipotoka tulipo na tunapoelekea

Naye katibu wa CCM wilaya ya Makete amesema utaratibu huo ulikuwa ni maazimio ya mkutano mkuu wa chama hicho wa mwaka jana, na utasaidia kuondoa upotoshwaji unaofanywa na vyama vya kisisa kuwa serikali haifanyi kazi

Mbali na hilo amesema ukimya wa baadhi ya watendaji wengi wa serikali ndiyo ulipelekea kutotolewa kwa taarifa hizi na hivyo utaratibu huu utasaidia wananchi kupata taarifa za maendeleo ya serikali yao

“Isifike sehemu uchaguzi ukaonekana ni sehemu nzuri ya kueleza serikali imefanya nini, hiyo siyo sahihi mi nadhani jukumu kubwa kama CCm ni kuendelea kuikumbusha serikali kutekeleza wajibu wake na tuachane na upotoshaji unaotolewa huko nje jamani tuupuuze” alisema Mtaturu

Mwenyekiti wa makanisa wilaya ya Makete Padri Haule amesema utaratibu huo pia utasaidia wao kama viongozi wa dini kwenda kuwaelezea wananchi mafanikio ya serikali hivyo serikali inatakiwa kuwapatia taarifa hizo ili wazitumie kuwaelewesha

Hata hivyo Sheikh wa wilaya ya Makete Anuari Sanga amesema utaratibu huo kwa kuwa unashirikisha wadau mbalimbali wanaofanya kazi na serikali ikiwemo viongozi wa dini, watapata fursa ya kuishauri na kutoa maoni yao pale wanaposomewa taarifa hiyo


JIUNGE NA EDMO BLOG SASA

Usipitwe!! Jiunge nasi kupitia Facebook,Twitter na Instagram ili kupata habari zote za town! Usikose kujiunga na Youtube kuangalia video zote kali kutoka Edmo Blog Pekee!, kujiunga bonyeza hapa>>>Youtube

Tupe Maoni Yako lakini Usiandike Matusi



 
© Copyright EDMO BLOG | Designed By Peruzibongo