DAR ES SALAAM, Tanzania
Kufuatia kuzuka maandamano na mijadala
kuhusu miradi ya utafutaji na uvunaji wa gesi nchini, Waziri wa Nishati na Madini Prof.
Mhongo (pichani) ameshuka mzima mzima na kutoa taarifa ndefu kwa umma
kufafanua mambo mbalimbali kuhusiana na sakata hilo. Mdau, Taarifa hii
tumeitoa kama tulivyoipata na ni hii ifuatayo:
1.0 UTANGULIZI
Wizara ya Nishati
na Madini inapenda kutoa ufafanuzi wa miradi ya Gesi Asilia ambayo
itatekelezwa kwa kushirikiana na wawekezaji katika Sekta ndogo ya Gesi
Asilia na kueleza manufaa makubwa yatakayopatikana kwa wananchi wote wa
Tanzania wakiwemo wale wa Mikoa ya Mtwara na Lindi.
Siku ya Alhamisi,
tarehe 27 Disemba 2012, baadhi ya Vyama vya Siasa vya Upinzani
viliratibu na kuhamasisha baadhi ya wakazi wa Mkoa wa Mtwara, wengi wao
wakitokea Mtwara Mjini kufanya maandamano ya kudai raslimali ya Gesi
Asilia iwanufaishe wakazi wa Mtwara na kupinga mradi mkubwa wa ujenzi
wa Bomba la Gesi Asilia kutoka Mtwara hadi Dar es Salaam. Wizara
ya Nishati na Madini inapenda kutoa taarifa ifuatayo kwa
Wa-Tanzania wote kwa kupitia vyombo vya habari.
Tokea Uhuru,
uchumi wa Tanzania umetegemea kilimo cha mazao ya biashara kama vile
katani (Tanga na Morogoro), pamba (Mwanza, Mara na Shinyanga), kahawa
(Kilimanjaro, Kagera, Ruvuma na Mara), chai (Iringa) na tumbaku
(Tabora). Fedha za mazao haya zimewanufaisha wakazi wa mikoa yote ya
nchi yetu bila ubaguzi wo wote wala wakulima wa kutoka mikoa hiyo
hawajawahi kufanya maandamano wakidai upendeleo (dhidi ya Wa-Tanzania wengine) wa
aina yo yote ile.
1 Mapato yatokanayo na
uchimbaji wa dhahabu (Mwanza, Geita, Mara, Shinyanga na Tabora), almasi
(Shinyanga) na tanzanite (Manyara) yamewanufaisha Wa-Tanzania wote bila
ubaguzi wo wote ule! Minofu ya samaki wa Ziwa Victoria (Mara, Mwanza na
Kagera) imeliingizia Taifa letu fedha nyingi ambazo zimetumiwa na
wakazi wa nchi nzima bila ubaguzi wo wote.
Aidha kuna mikoa
ambayo inazalisha mazao ya chakula kwa wingi kwa manufaa ya Wa-Tanzania
wote. Mahindi kutoka Rukwa, Mbeya, Ruvuma na Iringa yanasafirishwa
kwenda mikoa yote ya nchi yetu bila kujali eneo yanakolimwa na wakazi wa
mikoa hiyo hawajawahi kudai mahindi hayo ni kwa ajili ya watu wa
mikoa hiyo pekee. Sukari ya Kilombero, Mtibwa na Kagera inatumiwa na
wakazi wa mikoa yetu yote bila ya kuwepo madai ya mikoa inayozalisha
sukari hii kupewa upendeleo wa aina yo yote ile. Maji ya Mto Ruvu
yanatumiwa na wakazi wa Dar Es Salaam bila manung’uniko yo yote
kutoka kwa wakazi wa eneo la chanzo cha Mto Ruvu.
Umeme wa kutoka
Mtera, Kidatu na Kihansi (Dodoma na Morogoro), Hale (Tanga), na Nyumba
ya Mungu (Kilimanjaro) unatumiwa na wakazi wote wa Tanzania bila ubaguzi
au malalamiko ya wenyeji wa sehemu ambazo umeme huo unafuliwa na
kusafirishwa kwenye Gridi ya Taifa.
Kwa hiyo,
kutokana na mifano hii michache, ni wajibu wa wazalendo na wapenda
maendeleo wa kweli na hasa Wa-Tanzania wanaopinga ubaguzi wa aina yo
yote ile kujiuliza kwa kina sababu zilizopelekea Vyama Siasa vya
Upinzani kupanga, kuhamasisha, kushabikia na kuongoza maandamano ya tarehe 27
Disemba 2012 pale Mtwara Mjini.
KUSOMA ZAIDI BONYEZA HAPA