MSHTAKIWA KESI YA MZEE RUKSA ANAJUA SIRI NYINGI, ANADAI HAWEZI KUTOA MAHAKAMANI.

MTUHUMIWA anayedaiwa kumuibia rais mstaafu Ally Hassan Mwinyi sh.milioni 37, Abdallah Nassor Mzombe (40) zikiwa ni kodi ya pango katika nyumba mbili zinazomilikiwa na rais huyo, ameiambia mahakama ya Hakimu Mkazi Kisutu Dar es Salaam, kuwa anajua siri nyingi za Mwinyi ambazo kamwe hawezi kuzisema mahakamani hapo.

Mbele ya Hakimu Mkazi, Jenevitus Dudu, katika utetezi wake, mbali ya kukataa kutenda kosa hilo, Mzombe alidai amefanya kazi nyingi na kushirikishwa na mzee Mwinyi mambo mengi ya wazi na ya siri ambayo hata watoto wake wa kuzaa hawayajui na kwamba anashangazwa kuona sasa anashtakiwa kwa makosa ya kumuibia fedha hizo.


JIUNGE NA EDMO BLOG SASA

Usipitwe!! Jiunge nasi kupitia Facebook,Twitter na Instagram ili kupata habari zote za town! Usikose kujiunga na Youtube kuangalia video zote kali kutoka Edmo Blog Pekee!, kujiunga bonyeza hapa>>>Youtube

Tupe Maoni Yako lakini Usiandike Matusi



 
© Copyright EDMO BLOG | Designed By Peruzibongo