MAKAHABA 22 WAKAMATWA DAR ES SALAAM

Jeshi la Polisi nchini limewakamata zaidi ya wasichana 22 katika eneo la Mwananyamala karibu na geti la hospitali ya Mwananyamala akiwemo mama mtu mzima anayekadiliwa kuwa na umri wa miaka 70 ambaye alikuwa anamiliki jumba lenye zaidi ya vyumba 40 ambalo hutumika kufanyia ukahaba maarufu kama danguro.
Kamanda wa Polisi mkoa wa Kipolisi, Kinondoni, Kamanda Charles Kenyela  akizungumza na waandishi wa habari
Akitoa taarifa leo Kamanda wa Polisi Mkoa wa Kipolisi Kinondoni, Kamanda Charles Kenyela, amesema kuwa, wanashukuru wananchi ambao wameweza kutoa ushirikiano wa kukamatwa kwa wasichana hao ambao walikuwa wakifanya biashara ya ukahaba katika maeneo hayo kwa muda mrefu.
Mashuhuda wa tukio hilo, wamesema kuwa, wanalishukuru sana Jeshi Polisi kwa kuweza kuwakamata wasichana hao ambao wamekuwa wakifanya biashara hiyo ya ukahaba kwa muda mrefu.

Aidha mashuhuda hao wamesema kuwa, wasichana hao walikuwa wanafanya biashara hiyo kwa bei ya shilingi 2000, 3000 kwa muda mfupi (short time) na wateja wao ni vijana, akina baba pamoja na vijana ambao huwa wanabarehe kwa vile hawa huwa hawajui mapenzi huko huenda kufundishwa


JIUNGE NA EDMO BLOG SASA

Usipitwe!! Jiunge nasi kupitia Facebook,Twitter na Instagram ili kupata habari zote za town! Usikose kujiunga na Youtube kuangalia video zote kali kutoka Edmo Blog Pekee!, kujiunga bonyeza hapa>>>Youtube

Tupe Maoni Yako lakini Usiandike Matusi



 
© Copyright EDMO BLOG | Designed By Peruzibongo