IRINGA YAJA NA MIKAKATI YA KUPAMBANA NA UKIMWI NA DAWA ZA KULEVYA

 Mratibu msaidizi wa kudhibiti ukimwi mkoa wa Iringa akizungumza na waandishi wa habari kuhusu mikakati ya kudhibiti ukimwi na matumizi ya ukimwi
 naibu meya wa manispaa ya Iringa Gervas Ndaki akifungua mdahalo wa kudhibiti ukimwi na matumizi ya madawa ya kulevya

 mmoja wa wanafunzi Neema Magoma akichangia mada katika mkutano huo

Halmashauri ya Manispaa ya Mkoa wa Iringa imeandaa mikakati thabiti ya namna ya kupambana na  kuzuia maambukizi na matumizi ya dawa za kulevya  yanayozidi kuongezeka kwa kasi mkoani hapa.

Mwandishi Denis Mlowe anaripoti  kuwa hayo yamesemwa na Msaidizi wa Kudhibiti maambukizi ya virus vya ukimwi Gasper Nsanye wakati wa mdahalo ulioandaliwa na AMMICAL wa mpango wa majadiliano ya viongozi na wadau mbalimbali ulifanyika katika ukumbi wa hallfare na kuwashirikisha rika mbalimbali wakiwamo wanafunzi wa vyuo vikuu, sekondari na shule ya msingi na kufaidisha mkoa wa Iringa na wilaya za Temeke, Kinondoni na Ilala za Dar es Salaam.

Amesema kwamba mkoa wa Iringa umekumbwa na makundi matatu ambayo yamesaulika katika jamii kuhusiana na maambukizi  ya ukimwi na na matumizi ya madawa ya kulevya na ndio chanzo cha kuenea kwa kasi kubwa katika manispaa na kuifanya kuwa ya kwanza kitaifa kwa maambukizi ya ukimwi.“Lengo la kufanya mdahalo huu   ni juu ya athari za dawa za kulevya na ukimwi kuzuia na kudhibiti kabisa hadi kufikia hatua ya sufuri 3 katika kuenea kwa ukimwi, unyanyapaa na biashara ya madanguro na vijana wanaotumia madawa ya kulevya kufikia hatua ya sifuri 3” alisema Nsanye

Aidha amesema kwamba mkoa wa Iringa ni wa kwanza kitaifa ukiwa na asilimia 15.7 hivyo lengo  pia ni kuweka mikakati ya namna ya kukabiliana na vvu na ukimwi ili kupunguza vifo kufikia sifuri na kusaidia makundi hayo matatu ambayo ni baishara ya ngono,wanaojidunga madawa ya kulevya na wanaume wanaofanya mapenzi ya jinsi moja(ushoga).

Awali Naibu Meya wa Manispaa ya Iringa Gervas Ndaki amesema kwamba kwa sasa Iringa imeingiliwa na makundi hayo na ndio chanzo kikubwa cha kuenea kwa maambukizi katika manispaa na ni jukumu la kitu mwananchi kuweza kupambana na makundi haya kwa kuwapa elimu na kuweza kuwasaidia kuondokana na tabia hatarishi. “ Ni lazima tutokomeze haya makundi na  jamii yatakiwa kutambua kwamba makundi haya yapo na yanasababisha maambukiz makubwa ya virus vya ukimwi katika mkoa wa Iringa” amesema Ndaki.

Naye mwenzeshaji  Dr Jayson Mboya amesema kwamba kwa sasa watu milioni 33.3 wanaishi na virus vya ukimwi na wengi wao wako Kusini mwa Jangwa la Sahara ikiwemo Tanzania yenye watu milioni 1.6 na chanzo   kikubwa ni ngoni zembe zikiambatana na tabia hatarishi kama kujidunga madawa ya kulevya kwa kuazimana sindano, unywaji wa pombe kupita kiasi na wafungwa wanaofanya mapenzi ya jinsia moja.

Amesema jamii yatakiwa kuelimishwa kwa kiasi kikubwa madhara na athari ya utumiaji wa madawa ya kulevya  waweze kujiepusha na kutotumia kabisa aidha kuongezwa kwa vituo vya afya vitakavyohudumia waathirika wa madawa  kulevya  na vijana kujishughulisha na shughuli mbalimbali zikiwemo michezo.


JIUNGE NA EDMO BLOG SASA

Usipitwe!! Jiunge nasi kupitia Facebook,Twitter na Instagram ili kupata habari zote za town! Usikose kujiunga na Youtube kuangalia video zote kali kutoka Edmo Blog Pekee!, kujiunga bonyeza hapa>>>Youtube

Tupe Maoni Yako lakini Usiandike Matusi



 
© Copyright EDMO BLOG | Designed By Peruzibongo