CCM MAKETE YAPONGEZA WANANCHI KWA UJENZI WA BARABARA

Barabara ya Matamba - Nungu ambayo imetengenezwa kwa nguvu za wananchi

MC wa sherehe za mapinduzi akionesha wananchi kitita cha fedha zilizotolewa na CCM kuwaunga mkono wananchi hao kwa kujenga barabara hiyo

mwenyekiti wa CCM wilaya ya Makete Francis Chaula akizungumza na wananchi hao

Chama cha mapinduzi (CCM) wilayani Makete kimewataka wananchi wa Makete kutodanganywa na kuyumbishwa na mtu yeyote pindi wanaposhiriki katika shughuli za maendeleo katika wilaya yao

Hayo yamesemwa na mwenyekiti wa CCM wilaya ya Makete Bw. Francis Chaula wakati akitoa salamu za chama chake katika maadhimisho ya miaka 49 ya mapinduzi ya Zanzibar yaliyoadhimishwa kiwilaya katika kijiji cha Nungu kata ya Matamba

Amesema chama chake kimefarijika kuona wananchi waliyochangia nguvu zao katika kuchimba na kutengeneza barabara ya kutoka Matamba hadi Nungu, kwani hapo awali barabara hiyo haikuwepo na badala yake ilikuwa ni njia ya waenda kwa miguu, na kusema jambo hilo linafaa kuigwa na maeneo mengine wilayani hapo

Katika kuunga mkono jambo hilo mwenyekiti huyo alitoa fedha taslimu 50,000/= kama mchango wake wa kuunga mkono wananchi hao kutengeneza barabara hiyo huku wadau mbalimbali walioambatana naye katika maadhimisho hayo wakimuunga mkono kwa kumchangia mwenyekiti huyo na fedha hizo kufikia Tsh. 130,000/= fedha ambazo zilikabidhiwa kwa mtendaji wa kijiji hicho na kukatiwa risiti papo hapo

“Ndugu zangu hakuna mtu asiyependa maendeleo na kitendo mlichokifanya wana nungu mimi kama mwenyekiti wa CCM, tumefarijika sana na ndio maana mmeona wenzangu walivyoniunga mkono na kuchanga 130,000/= ni kwa kuwa watu wanakipenda chama cha mapinduzi nawaombeni fanyeni maendeleo achaneni na propaganda na hao wengine wanaokuja kuwadanganya hapa” alisema

Hatua iliyobakia hivi sasa kwenye barabara hiyo ni uwekaji wa kifusi ili isiteleze na iendelee kutumika kwa muda mrefu na fedha hizo zilizochangwa moja ya kazi zake ni kusaidia uwekaji wa kifusi


JIUNGE NA EDMO BLOG SASA

Usipitwe!! Jiunge nasi kupitia Facebook,Twitter na Instagram ili kupata habari zote za town! Usikose kujiunga na Youtube kuangalia video zote kali kutoka Edmo Blog Pekee!, kujiunga bonyeza hapa>>>Youtube

Tupe Maoni Yako lakini Usiandike Matusi



 
© Copyright EDMO BLOG | Designed By Peruzibongo