APIGA PICHA AKIWA KABEBA MOYO WAKE BAADA YA UPASUAJI

Penny akiwa kashikilia moyo wake kwa mikono yake mwenyewe baada ya upasuaji.
Mgonjwa aliyepandikizwa kiungo amepigwa picha akiwa kashikilia moyo wake mwenyewe kwa mikono yake baada ya kunusurika kufa kwa saratani na viungo kushindwa kufanya kazi.

Pamoja na kufichwa sehemu kubwa ya uso wake kwa kofia maalumu ya matibabu, macho ya Penny yanaonekana bayana huku moyo wake mpya ukidunda kifuani mwake na akiwa amebeba moyo wake wa zamani kwa mara yake ya mwisho kufuatia mafanikio ya upasuaji aliofanyiwa.

Rafiki wa Penny, Kelsey alituma picha kwenye ukurasa wake wa Imgur akisema: "Penny akiwa amebeba moyo wake mwenyewe. Amenusurika saratani na moyo wake kushindwa kufanya kazi na hakuwahi kukata tamaa."
Kwa mujibu wa maelezo ya Kelsey, madaktari walimruhusu Penny kupiga picha akiwa kabeba moyo wake uliokufa kabla haujachomwa moto.

Akiwa kauzingira wote mikono yake, ameuinua moyo huo karibu na kamera kama vile alikuwa kabeba tuzo.
Sasa picha ya afya njema, anayo picha hii kama ukumbusho wa mateso na kumbusho la jinsi alivyokuwa na bahati kuweza kuwekewa moyo mpya.


 


JIUNGE NA EDMO BLOG SASA

Usipitwe!! Jiunge nasi kupitia Facebook,Twitter na Instagram ili kupata habari zote za town! Usikose kujiunga na Youtube kuangalia video zote kali kutoka Edmo Blog Pekee!, kujiunga bonyeza hapa>>>Youtube

Tupe Maoni Yako lakini Usiandike Matusi



 
© Copyright EDMO BLOG | Designed By Peruzibongo