AMANDA WA BONGO MOVIE AMTAMBULISHA "BWANA MISOSI" KWA WAZAZI WAKE


MWIGIZAJI wa sinema za Kibongo, Tamrina Mohamed ‘Amanda’ amemtambulisha mume wake mtarajiwa, staa wa Bongo Fleva, Joseph Rushau ‘Bwana Misosi’ kwa wazazi wake.

Tukio hilo lilichukua nafasi mwishoni mwa wiki iliyopita pande za Msasani Beach, jijini Dar wakati mwigizaji huyo alipokuwa akiadhimisha siku yake ya kuzaliwa, ndipo alipotumia nafasi hiyo kumtambulisha Bwana Misosi kwa mama yake mzazi na mjomba wake.

“Kula keki na kunywa shampeni pamoja na mama yangu, mjomba, mama Dotnata na wageni waalikwa ni ishara tosha kwamba Misosi umekubalika katika familia yetu, jisikie uko nyumbani,” alisikika Amanda.

Katika shughuli hiyo, Amanda alimuandalia mpenzi wake huyo ambaye ni mwanamuziki keki maalum yenye muonekano wa gitaa kama ishara ya upendo kwake.


JIUNGE NA EDMO BLOG SASA

Usipitwe!! Jiunge nasi kupitia Facebook,Twitter na Instagram ili kupata habari zote za town! Usikose kujiunga na Youtube kuangalia video zote kali kutoka Edmo Blog Pekee!, kujiunga bonyeza hapa>>>Youtube

Tupe Maoni Yako lakini Usiandike Matusi



 
© Copyright EDMO BLOG | Designed By Peruzibongo