WALIMU NA WANAFUNZI SHULE YA MSINGI LIPANGALA WAJISAIDIA PORINI , MBUNGE FILIKUNJOMBE AGEUKA MBOGO

Hiki ni  choo cha  muda  cha kwanza  cha shule ya msingi Lipangala Ludewa mkoani Njombe    kilichobomoka toka mwaka 2004


 Hiki ni choo cha kisasa ambacho  kimejengwa  sasa katika  shule ya Msingi Lipangala ambacho pia kimeanza kubomoka
 Hiki kilikuwa ni choo cha  walimu miaka  hiyo kwa  sasa shimo jipya  linachimbwa mbele  ili  kurejesha huduma ya choo kwa  walimu
 Hii ndilo hali halisi ya  choo hiki cha  walimu shule ya Msingi Lipangala Ludewa ,kwa  sasa hakitumiki
Mbunge Filikunjombe akiagiza choo kujengwa haraka 

Na Francis Godwin Blog
WAKATI serikali  kupitia wizara ya elimu  na mafunzo ya ufundi ikiendelea kuweka mikakati ya  kuboresha  elimu ya awali na msingi  ,mbunge  wa  jimbo la Ludewa  Deo Filikunjombe asikitishwa na shule  ya msingi Lipangala  wilaya Ludewa mkoani Njombe kukosa choo cha walimu na wanafunzi na kupelekea walimu  wa shule hiyo kuendelea kujisaidia vichakani kwa zaidi ya miaka  5 hivi  sasa  .

Kutokana na shule  hiyo kukosa vyoo  vya  wanafunzi na walimu mbunge huyo aagiza uongozi  wa kata hiyo pamoja na tarafa kuhakikisha  wanakamilisha  ujenzi  vyoo ndani ya  siku 10  kunzia juzi na pindi  shule zitakapofungua kuwepo na vyoo vya uhakika shuleni hapo.

Wakizungumza katika  mkutano  wa  mbunge Filikunjombe wananchi  wa kijiji  cha Lipangala   walisema  kuwa  wnasikitishwa  kuona  walimu  wa shule  hiyo  wakikimbi kwenda kujisaidia vichakani  huku baadhi yao  wakilazimika  kwenda  majumbani kwao kupata  huduma ya choo jambo ambalo wmedai ni hatari katika maendeleo ya  elimu shuleni hapo.

Saraha Edward alisema   kuwa mbali  ya  walimu  kuendelea kufundisha shule  hiyo  bila ya  choo bado  wanafunzi   wamekuwa wakipata tabu kubwa kupata  huduma  ya choo kutokana n vyoo vilivyokuwepo shuleni hapo kuwa na hali mbaya  zaidi.

"Hii shule  yetu ni vema ikafungwa kabisa  kwani tunawasiwasi mkubwa  watoto wetu  kuja kupatwa na magonjwa ya mlipuko kutokana na shule kutokuwa na  choo cha uhakika ni kama  wanajisaidia porini kwani hivi si vyoo vya kujivunia kama shule"

Mmoja kati ya  walimu wa  shule  hiyo ambae hakupenda  kutaja jina lake kwa  kuwa  si msemaji wa shule  hiyo alisema  kuwa  shule  hiyo imekuwa  ikiendeshwa  bila choo toka mwaka 2004 ambapo wanafunzi walianza kukosa choo cha uhakika baada ya  kile kilichokuwepo awali kubomoka .

Kutokana na tatizo hilo la choo  cha  wanafunzi  kubomoka  wananchi  walilazimika   kujenga choo cha muda ambacho pia hakikuchuku muda kilibomoka na hivyo kuendelea kushirikiana choo kimoja na  walimu kwa  kipindi cha mwaka mmoja na baada ya hao hata choo cha walimu  pia kilibomoka hivyo  kukosa choo cha  walimu na kulazimika kujenga choo cha muda ambacho ni hatari  pia  kwa usalama  wa wanafunzi huku walimu  wao wakilazimika kwenda kupata  huduma  hiyo majumbani kwao ama porini .

Uchunguzi   uliofnywa na mwandishi  wa  habari hizi  shuleni hapo umebaini  kuwa  choo cha  walimu  chenye matundu mawili  kilichokuwepo awali kimekuwa hakitumiki  toka  mwaka 2005  kutokana na choo hicho  kubomoka  kutokana na kujengwa  chini ya  kiwango pasipo kujengewa saruji  huku  ardhi  ya eneo hilo ikiwa inaongoza kwa  kuwa na unyevu unyevu.

Afisa tarafa  ya Liganga Edward Wayotile alithibitisha madai  hayo ya  shule  kuendeshwa  bila  choo na  kuwa tayari  wameweka mkakati  wa  kujenga vyoo katika  shule  hiyo .

Alisema  kuwa mkakati ni kujenga vyoo  vipya vyenye matundu 16 kwa  wavulana na matundu 12 kwa wasichana  pamoja na kujenga choo chenye matundu mawili kwa ajili ya  walimu  wa  shule  hiyo.

Kwa  upande  wake mbunge  wa  jimbo  hilo la Ludewa Bw Filikunjombe mbali ya  kueleza masikitiko yake juu ya shule  hiyo  kukosa vyoo bado aliuagiza  uongozi  wa kata ,tarafa na wilaya  kufika mara moja katika  shule  hiyo  ili  kujenga choo hicho ndani ya siku 11 kuanzia juzi ili  wanafunzi  watakapoanza masomo  kuwepo kwa huduma ya uhakika ya choo cha  wanafunzi na  walimu.

"Haiwezekani shule  kuendeshwa  bila vyoo ....sasa naomba  viongozi  wa  elimu wilaya  kushughulikia tatizo hilo mara moja  kwani  kama tutaacha suala  hilo ni  kutoitendea haki elimu ya watoto wetu"

Mbunge  Filikunjombe  pia alikabidhi msaada  wa bati 50 kwa diwani  wa kata  hiyo kwa ajili ya ukamilishaji  wa darasa la awali katika  shule  hiyo  huku akimuagiza mkurugenzi mtendaji  wa Halmashauri ya  wilaya ya  Ludewa  kutoa fedha katika mfuko  wa maafa kwa ajili ya ujenzi wa vyoo kwenye  shule  hiyo.

Wakati  huo huo  mbunge  huyo  aliwataka   wazizi  wenye  watoto waliofaulu  kujiunga na  elimu  ya sekondari  mwakani kuhakikisha wanafanya maandalizi mapema na kutotumia fedha zote katika sherehe za  kufunga mwaka na kuacha  kutenga  fedha kwa ajili ya kusomesha   watoto sekondari.


JIUNGE NA EDMO BLOG SASA

Usipitwe!! Jiunge nasi kupitia Facebook,Twitter na Instagram ili kupata habari zote za town! Usikose kujiunga na Youtube kuangalia video zote kali kutoka Edmo Blog Pekee!, kujiunga bonyeza hapa>>>Youtube

Tupe Maoni Yako lakini Usiandike Matusi



 
© Copyright EDMO BLOG | Designed By Peruzibongo