NYUKI WALETA KIZAAZAA MSIBANI

MWENYEKITI wa Halmashauri wa Wilaya ya Moshi Vijijini, Morris Makoyi juzi alilazimika kuongoza mamia ya waombolezaji kutimua mbio kuokoa roho zao, baada ya kushambuliwa na kundi la nyuki msibani.
 
Tukio hilo la aina yake na lisilo la kawaida, limetokea baada ya kuzikwa marehemu Agnes Malya aliyekuwa na umri wa miaka 30, ambaye inadaiwa ameacha wosia kuwa kusiwe na mbwembwe kama vile vyakula, pombe, suti na sare nyingine wakati wa mazishi yake.
 
 Katika mbio hizo, Makoyi aliongozana na Paroko wa Parokia ya Mkombole, aliyefahamika kwa jina moja la Ephraim waliacha magari ya kifahari waliyofika nayo msibani na kukimbilia migombani.
 
Nyuki hao, wakiwa katika makundi makubwa matano walijitokeza na kuanza kuwashambulia waombolezaji, baada ya mazishi ya marehemu Malya aliyezikwa katika Kijiji cha Osaki huku tukio hilo, likihusishwa na madai ya kupuuzwa kwa wosia wa marehemu ambaye alipinga kuandaliwa vyakula na vinywaji, vitu ambavyo vitagharimu fedha ambazo zingetosha kugharamia matibabu yake, kutokana na ugonjwa wa kansa ya ziwa uliogharimu maisha yake.

 Kutokana na kizaazaa hicho, chakula na vinywaji vyenye thamani ya zaidi ya Sh milioni 5, vinasemekana vilimwagwa kama ishara ya kutimiza alichokisema marehemu Agnes. Lakini hilo lilifanyika baada ya nyuki kuwakimbiza waombolezaji.


JIUNGE NA EDMO BLOG SASA

Usipitwe!! Jiunge nasi kupitia Facebook,Twitter na Instagram ili kupata habari zote za town! Usikose kujiunga na Youtube kuangalia video zote kali kutoka Edmo Blog Pekee!, kujiunga bonyeza hapa>>>Youtube

Tupe Maoni Yako lakini Usiandike Matusi



 
© Copyright EDMO BLOG | Designed By Peruzibongo