MSANII WA FILAMU AFUNGUKA "TANGU SHARO MILIONEA AFE PRESHA IMEKUWA IKINISUMBUA"


HALI ya msanii kiwango wa filamu za Kibongo, Snura Mushi ‘Snura’ siyo nzuri kufuatia kusumbuliwa na ugonjwa wa Moyo.

Akizungumza na paparazi wetu aliyemtembelea msanii huyo hivi karibuni nyumbani kwake, Mwananyamala, Dar es Salaam baada ya kupata taarifa ya kuumwa kwake, msanii huyo alisema anaumwa sana.
Msanii huyo alisema kuwa, kadiri siku zinavyokwenda ndivyo maradhi hayo yanazidi kumshambulia.

Aliongeza kwamba, tatizo hilo lilimuanza alipokwenda  Muheza, Tanga kuhudhuria msiba wa Hussein Ramadhan Mkieti ‘Sharo Milionea’.

“Yaani sina hamu ya kula, kutapika ndiyo huku, sijui ni hizi dawa za malaria nilizomeza ndiyo zinasababisha hali hii,  naumwa sana jamani...niombeeni kwa Mungu nipone,” alisema Snura.
 
BIG UP MPEKUZI BLOG


JIUNGE NA EDMO BLOG SASA

Usipitwe!! Jiunge nasi kupitia Facebook,Twitter na Instagram ili kupata habari zote za town! Usikose kujiunga na Youtube kuangalia video zote kali kutoka Edmo Blog Pekee!, kujiunga bonyeza hapa>>>Youtube

Tupe Maoni Yako lakini Usiandike Matusi



 
© Copyright EDMO BLOG | Designed By Peruzibongo