FACEBOOK YATISHIA KUJITOA ENDAPO HATUTAKUBALI "USHOGA"



Huenda Facebook ikafikia uamuzi wa kuichijia baharini Uganda katika orodha ya nchi inakopatikana kutokana na msimamo mkali wa nchi hiyo dhidi ya mashoga.

Hivi karibuni Uganda imejikuta kwenye kiti moto kutokana na msimamo wake kwa mashoga huku wabunge wakipanga kupitisha muswada wa sheria dhidi ya ushoga ambayo itakuwa na adhabu kali kwa jamii hiyo.
Hatua hiyo imezifanya baadhi ya nchi wahisani kutishia kuweka vikwazo vya kifedha na usafiri kwa viongozi walio mstari wa mbele kukandamiza haki za mashoga nchini Uganda.

Inadaiwa kuwa mwanzilishi wa Facebook, Mark Zuckerberg atatoa tamko rasmi kuhusiana na Uganda.


Kama hatua hiyo ikichukuliwa makampuni mengi yanayotafuta kujijenga kupitia mtandao huo wa kijamii yataathirika vibaya.
 
SOURCE: MPEKUZI


JIUNGE NA EDMO BLOG SASA

Usipitwe!! Jiunge nasi kupitia Facebook,Twitter na Instagram ili kupata habari zote za town! Usikose kujiunga na Youtube kuangalia video zote kali kutoka Edmo Blog Pekee!, kujiunga bonyeza hapa>>>Youtube

Tupe Maoni Yako lakini Usiandike Matusi



 
© Copyright EDMO BLOG | Designed By Peruzibongo