REDIO ZATAKIWA KUZIDI KUBORESHA VIPINDI VYAKE


Redio zilizopo mikoa mbalimbali hapa nchini zimetakiwa kuboresha vipindi vyao ili viendelee kuvutia wasikilizaji pamoja na kuzidi kuwaelimisha zaidi

Rai hiyo imebainika wakati vituo 10 vya redio vinavyofanya kazi kwa kushirikiana na Johns Hopkins University Centre for Comuunication Programs (JHU-CCP) vilipokutana hii leo kwenye hoteli ya Top Life iliyopo mkoani Morogoro

Wakizungumza wakati wa warsha hiyo watangazaji na waandaji hao wa vipindi wamesema, kudaiwa malipo wakati wa kufanya vipindi ni moja ya changamoto kubwa wanayokumbana nayo inyopelekea vipindi vyao kupwaya kwa kuwa hawana fedha za kuwalipa

“Unajua hili ni tatizo kubwa, wataalamu wengi wanadhani tuna fedha za kuwalipa, lakini wanasahau kuwa wao ni kioo cha jamii pia wanatakiwa kutusaidia kuwapa ufafanuzi wasikilizji wetu kuhusiana na mada mbalimbali kwani wao ndio wataalamu wenyewe, lakini pia wananchi nao wanatakiwa kutoa taarifa tu bila kudai malipo, sisi hatuna hela” alisema Jumanne Juma mtangazaji wa Nuru FM mkoani Iringa

Vituo kumi vya redio ambavyo ni Nuru FM, Ebony FM, Uplands FM, Kitulo FM, Bomba FM, Radio Free Africa, Voice Of Tabora, Victoria FM, Uhuru Fm na Radio One Stereo ni vituo ambavyo vimekuwa vikifanya kazi na JHU-CCP kutoa elimu kuhusiana na mambo mbalimbali ikiwemo VVU/UKIMWI ambapo pia kwa hivi sasa Clouds FM, Times FM na Best FM ni vituo ambavyo vimeongezwa kufanya kazi pia na shirika hilo

Mafunzo hayo yanalenga kuboresha vipindi hivyo na kuvifanya viwe bora zaidi na kuzidi kuwavutia wasikilizaji wa redio hizo


JIUNGE NA EDMO BLOG SASA

Usipitwe!! Jiunge nasi kupitia Facebook,Twitter na Instagram ili kupata habari zote za town! Usikose kujiunga na Youtube kuangalia video zote kali kutoka Edmo Blog Pekee!, kujiunga bonyeza hapa>>>Youtube

Tupe Maoni Yako lakini Usiandike Matusi



 
© Copyright EDMO BLOG | Designed By Peruzibongo